logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matiang'i aondoka makao makuu ya DCI baada ya kuhojiwa kwa saa kadhaa

Matian'gi aachiliwa na DCI baada ya kuhojiwa.

image
na

Makala07 March 2023 - 13:46

Muhtasari


• Viongozi wa Azimio akiwemo Eugene Wamalwa waliandamana naye katika makao makuu ya DCI.

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiang'i akiwa nje ya makao makuu ya DCI Jumanne, Machi 7, 2023. Picha: ENOS TECHE

Aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang'i hatimaye ameondoka makao makuu ya DCI baada ya kuhojiwa kwa muda wa saa nane.

Matiang'i alifika katika makao makuu ya DCI muda wa saa mbili  asubuhi siku ya Jumanne.

Hapo awali,kiongozi wa Azimio Raila Odinga aliwasili ili kuungana naye lakini alizuiliwa kuingia alipofika langoni.

 

Mawakili wa Matiang’i walikuwa wamesema kwamba mteja wao angewasili katika makao makuu ya DCI mwendo wa saa mbili, saa moja kabla ya muda aliyoelekezwa.

Wakili wake Danstan Omari alisema kwamba alimwandikia afisa wa mwaliko kumjulisha kuhusu mabadiliko hayo.

 

"Tunathibitisha kuwa tutakuwepo, hakuna chochote cha kuficha," alisema.

 

Matiang'i alikuwa anatakiwa kuhojiwa kuhusiana na madai ya polisi kuvamia nyumba yake huko Karen usiku wa Februari 8.

Polisi na idara zote za usalama walikanusha kuhusika na uvamizi huo wakidai kuwa uzushi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved