logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ushoga ni dhambi-Muhoozi asema huku akishauri mataifa ya Afrika

Muhoozi Kainerugaba amechagua kutoa mwongozo kwa mataifa ya Afrika.

image
na Radio Jambo

Makala07 March 2023 - 11:45

Muhtasari


  • Muhoozi amefahamisha mataifa ya Afrika kwamba, kwa ujumla wake, anapendelea amani kuliko migogoro
KWA HISANI

Jenerali Muhoozi Kainerugaba kwa mara uya kwanza ametoa maoni yake kuhusu uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu LGBTQ.

Muhoozi Kainerugaba amechagua kutoa mwongozo kwa mataifa ya Afrika.

Kainerugaba ameshauri dhidi ya ushoga, akiitaja kuwa ni tabia ya dhambi.

Jenerali huyo kutoka Uganda pia amesema kuwa ushoga ni kinyume na Biblia jinsi inavyofundisha.

Hakuna kitu kitamu duniani, kulingana na jenerali wa Uganda, kuliko mwanamke.

Kulingana na Muhoozi, janga linakumba mataifa ya Afrika. Ameeleza kuwa hawezi kuruhusu ushoga katika bara la Afrika katika ushauri wake kama kamanda mkuu wa jeshi la Uganda.

Muhoozi amefahamisha mataifa ya Afrika kwamba, kwa ujumla wake, anapendelea amani kuliko migogoro.

Muhoozi anasisitiza kwamba bara la Afrika lina nguvu kweli kweli na kwamba baadhi ya mila, kama vile ushoga, hazifai kuvumiliwa.

"Kuna janga limezikumba nchi zetu... linaua watoto wetu. Kama Jenerali Mkuu wa Kiafrika, lazima niseme na kuwashauri. Ushoga ni DHAMBI! Mwenyezi Mungu aliwakusudia wanaume tu kwa wanawake na kinyume chake. Hakuna kitu kitamu zaidi ya mwanamke hapa duniani."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved