logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maswali ya Azimio kwa Ruto kuhusu 'kushindwa kurekebisha uchumi'

walisema kile ambacho Rais William Ruto amekuwa akifanya ni kutoa visingizio.

image
na Radio Jambo

Habari08 March 2023 - 12:22

Muhtasari


  • Walisema mkuu wa nchi pia amekuwa akisogeza ratiba zake alizoziweka kuhusu ahadi muhimu alizotoa kwa watu wa Kenya
  • Waliongeza kuwa ikiwa hawatapata majibu ya maswali, hawatakuwa na chaguo ila kuingia mitaani

Viongozi wa muungano wa Azimio waliochaguliwa Jumatano walimkashifu Rais William Ruto kwa kukosa kutimiza ahadi yake ya kampeni, miezi saba baada ya kuchukua mamlaka.

Wabunge hao wakiongozwa na kiongozi wa Wachache na Kinara wa Seneti, Enock Wambua na Edwin Sifuna walisema kile ambacho Rais William Ruto amekuwa akifanya ni kutoa visingizio.

Walisema mkuu wa nchi pia amekuwa akisogeza ratiba zake alizoziweka kuhusu ahadi muhimu alizotoa kwa watu wa Kenya.

“Maswali yetu kwa William Ruto, Gachagua, timu ya Hazina ya Kitaifa na lile linalojiita baraza la washauri wa masuala ya kiuchumi ni:

  • Je, mambo yatakuwa bora lini?
  • Je, ni lini shilingi itaacha kuanguka na kupoteza fedha nyingine?
  • Je, uhaba wa dola utaisha lini?
  • Je, ni lini bei ya bidhaa muhimu itashuka?
  • Mpango ni nini?
  • Je, mpango huo unaweza kushirikiwa na Wakenya?

Wabunge hao wa Upinzani walibaini kuwa Ruto aliahidi kupunguza gharama ya maisha lakini hilo linasalia kuwa ndoto.

Waliongeza kuwa ikiwa hawatapata majibu ya maswali, hawatakuwa na chaguo ila kuingia mitaani.

"Kisha tukaambiwa Kenya ilikuwa na leseni ya vyakula vya GMO. Bado, bei ilikataa kushuka na uchumi ukakataa kuimarika. Kisha tukaambiwa tusubiri kwa miezi sita. Kila miezi inapofika, malengo yanabadilika tena."

"Tunataka majibu na wasipokuja siku chache zijazo, hatutakuwa na namna zaidi ya kuwaongoza wafuasi wetu kuingia katika ofisi hizi ili kupata majibu. Tutawafuata maofisa hawa popote pale ili kupata majibu na si maonyo."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved