logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa watatu wakamatwa kwa madai ya kuuza mechi

"Shirikisho linapenda kuwashukuru polisi na baadhi ya wachezaji wa Ligi Kuu ya FKF

image
na Radio Jambo

Habari11 March 2023 - 13:29

Muhtasari


  • Shirikisho la Soka la Kenya, katika taarifa iliyotiwa saini na Afisa Mkuu Mtendaji Barry Otieno, liliwashukuru polisi kwa usaidizi wao

Mkenya mmoja na raia wawili wa kigeni mmoja wa Urusi na mwingine wa Uganda wanaodaiwa kutoa hongo na upangaji matokeo wamekamatwa na polisi.

Shirikisho la Soka la Kenya, katika taarifa iliyotiwa saini na Afisa Mkuu Mtendaji Barry Otieno, liliwashukuru polisi kwa usaidizi wao na kuahidi kulinda uadilifu wa soka ya Kenya.

"Shirikisho linapenda kuwashukuru polisi na baadhi ya wachezaji wa Ligi Kuu ya FKF waliosaidia kukamatwa na kuzuiliwa kwa watu watatu, miongoni mwao Mkenya na raia wawili wa kigeni," taarifa hiyo ilisema kwa sehemu.

"FKF inaendelea kufanya kazi kwa karibu na wote wanaohusika, ikiwa ni pamoja na vyombo vya usalama vya ndani na kimataifa, sio tu kusaidia katika mashtaka ya washukiwa waliotajwa lakini pia katika jitihada zinazolenga kulinda uadilifu wa soka la Kenya."

Inabainisha FKF imeanzisha kwa usaidizi wa FIFA na vilabu vya ndani mfumo wa kina ili kusaidia katika kugundua, kuzuia na kuripoti shughuli za udanganyifu wa mechi.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved