logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wachezaji wawili wa kandanda wauawa kwa kupigwa na radi Kisii

Wachezaji wengine wawili wanauguza majeraha katika Hospitali ya Rufaa ya Nyamira ambapo walikimbizwa kwa matibabu.

image
na

Makala13 March 2023 - 04:09

Muhtasari


•Timu hizo - Manyansi na Nyagiti- zilikuwa zikicheza mechi ya kirafiki wakati wa tukio hilo la saa kumi unusu alasiri.

•Mchezaji mmoja alifariki katika eneo la tukio huku wa pili akifariki akiwa hospitalini ambako alikimbizwa kwa matibabu ya dharura.

Rip

Wasimamizi wa kandanda katika eneo la Kitutu Chache, Kisii, wanasema kuwa wachezaji wawili wa kandanda waliuawa na radi wakati wa mechi iliyokuwa ikiendelea kwenye uwanja wa Manyansi.

Timu hizo - Manyansi na Nyagiti- zilikuwa zikicheza mechi ya kirafiki wakati wa tukio hilo la saa kumi unusu alasiri.

Waliofariki walitambuliwa kuwa ni Sammy Musa, 20, na Joshua Nyangaresi, 21.

OCPD wa Marani, Benlife Munuve, alisema mchezaji mmoja alifariki katika eneo la tukio huku wa pili akifariki akiwa hospitalini ambako alikimbizwa kwa matibabu ya dharura.

Evans Akanga, Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka la Kaskazini la Kitutu Chache, alisema wachezaji hao walifariki Jumamosi jioni wakati wa mchuano wa kirafiki.

Wachezaji wengine wawili wanauguza majeraha katika Hospitali ya Rufaa ya Nyamira ambapo walikimbizwa kwa matibabu.

"Timu zilikuwa na mechi ya kirafiki wakati mvua ilianza kunyesha ghafla," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved