logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume ashambuliwa na tembo aliyetoroka hifadhi wakati anajipiga ‘selfie’ naye

Migogoro kati ya binadamu na wanyamapori ni jambo la kawaida nchini Tanzania,

image
na Radio Jambo

Habari14 March 2023 - 13:58

Muhtasari


  • Kamishna wa polisi wa eneo hilo alisema tembo hao walikasirika na kuanza kuchanganyikiwa baada ya kundi la wenyeji kuwakaribia na kuanza kupiga selfie nao.

Mwanaume mmoja raia wa Tanzania yuko katika hali mbaya hospitalini baada ya kujipiga picha yaani ‘selfie’ na tembo yaani ndovu kabla ya kumgeukia na kumshambulia.

Ni sehemu ya kundi la wanyama waliotoroka eneo la hifadhi katika mkoa wa Manyara kaskazini na kula mazao ya shambani katika kijiji kimoja, kwa mujibu wa mamlaka.

Kamishna wa polisi wa eneo hilo alisema tembo hao walikasirika na kuanza kuchanganyikiwa baada ya kundi la wenyeji kuwakaribia na kuanza kupiga selfie nao.

“Mtu huyo amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Kiteto na anaendelea na matibabu...hali yake imeimarika kidogo,” alisema George Katabazi.

Migogoro kati ya binadamu na wanyamapori ni jambo la kawaida nchini Tanzania, ambapo vipindi vya ukame mara nyingi husababisha wanyamapori kukimbilia mashambani kutafuta chakula.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved