logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alichosema Kioni kuhusu maandamano ya Azimio

Mrengo wa Azimio ulifanya maandamano kkwenye kaunti tofauti siku ya Jumatatu.

image
na Radio Jambo

Makala20 March 2023 - 14:08

Muhtasari


  • Kulingana naye hawatakubali shinikizo kutoka kwa serikali ya rais William Ruto ili kusitisha maandamano hayo.

Katibu Mkuu wa Jubilee Jeremiah Kioni amejibu kupitia ukurasa wake rasmi wa twitter kuhusu Maandamano ya Azimio yanayoendelea katika kaunti ya Nairobi na katika baadhi ya kaunti tofauti nchini.

Kulingana naye hawatakubali shinikizo kutoka kwa serikali ya rais William Ruto ili kusitisha maandamano hayo.

"Maandamano ya amani ya kulinda mustakabali wa taifa letu yako kwenye TRACK. Wetu ni msimamo wa UTHUBUTU wa Usawa wa Kiuchumi kwa WAKENYA wote.Hatutaghairi katika vita hii ya UKWELI na HAKI YA KIJAMII."

Mrengo wa Azimio ulifanya maandamano kkwenye kaunti tofauti siku ya Jumatatu.

Huku maandamano yakiwa yameshika kasi baadhi ya wanasiasa na waandamanji walitiwa mbaroni.

Kinara wa Azimio Raila Odinga alitishia kumshtaki Rais Ruto kwa madai kwamba amevunja sheria.

Raila aliandamana na Kalonzo Musyoka,Ledama Ole Kina,Martha Karua,Makau Mutua,Babu Owino,Gladys Wanga,Peter Salasya miongoni mwa viongozi wengine.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved