logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maandamano yatafanyika kila Jumatatu - Raila Odinga

Kalonzi pia aliwataka polisi kutokubali kutumika vibaya akisisitiza maandamano hayo ni ya amani.

image
na Radio Jambo

Makala20 March 2023 - 12:22

Muhtasari


• Katika msafara huo, Odinga aliandamana na wanachama wengine akiwemo Kalonzo Musyoka, Martha Karua na Eugene Wamalwa.

Kinara wa Azimio la Umoja One Kenya Raila Odinga ametangaza wazi kwamba maandamano dhidi ya serikali ya rais William Ruto yatakuwa yakifanyika kila Jumatatu mpaka wakati matakwa yao yatakaposikilizwa na serikali ya rais Ruto.

Odinga alizungumza katika mtaa wa Eastleigh Nairobi ambako msafara wake ulielekea baada ya kuzuiliwa kuingia maeneo ya katikati mwa jiji na maafisa wa polisi ambao waliwatupia vitoa machozi.

Odinga alisema kwamba wana matakwa matatu ambayo wanataka serikali ya Ruto kutii ikiwemo kufunguliwa kwa seva za tume ya uchaguzi na mipaka IEBC, kupunguzwa kwa gharama ya maisha na kusitishwa kwa shughuli ya kuwateua makamishna wa IEBC - shughuli ambayo inasimamiwa na rais Ruto.

Odinga alisema kwamba shughuli hiyo ya kuwateua makamishna hao inafaa kuwajumuisha watu kutoka mirengo yote na wala sio mrengo wa serikali.

Katika msafara huo, Odinga aliandamana na wanachama wengine akiwemo Kalonzo Musyoka, Martha Karua na Eugene Wamalwa.

Msafara huo ulitafuta njia mbadala baada ya kuzuiliwa kuingia katikati mwa jiji kutoka barabara ya Kenyatta ambapo walizunguka jiji na kuingia Kamukunji ambapo Odinga aliwahutubia wafuasi wake kwa muda mfupi kabla ya kuelekea maeneo ya Pangani kuingia Eastleigh.

Kalonzo alipokuwa anazungumza, polisi walirusha vitoa machozi na kusambaratisha hotuba yake ambapo msafara huo ulilazimika kuondoka na kwendelea na ziara yao katika mtaa huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved