logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto achukua mikopo 8 ndani ya miezi 4

Serikali ya Rais Ruto imechukua jumala ya mkopo ya shilingi bilioni 43 ndani ya miezi minne.

image
na Radio Jambo

Habari24 March 2023 - 06:07

Muhtasari


• Hazina inaeleza kuwa mikopo hiyo itatumika kugharamia miradi ya maji, usalama wa chakula, afya ya uzazi, uboreshaji wa sekta isiyo rasmi na Biashara Ndogo na za Kati (MSMEs).

Utawala wa Kenya Kwanza tayari ilipokea mikopo minane  ya thamani ya shilingi bilioni 43.4 katika muda wa miezi minne, kati ya Septemba 1 hadi Desemba 31.

Hazina ya kitaifa inasema mikopo mipya iliyotiwa saini kati ya serikali ya Kenya, na wakopeshaji italipwa kati ya mwaka wa 2030 na 2047.

“Jumla ya thamani ya mikopo minane iliyosainiwa ni sawa na  shilingi bilioni 43,381, 450,293. Miwili kati ya mikopo hiyo ilikuwa imetolewa wakati wa kuwasilisha ripoti hii,” Njuguna Ndungu, waziri wa fedha aliambia wabunge. 

Serikali ya Rais Ruto inategemea mikopo ya masharti nafuu kugaramia mikopo ghali ya muda mfupi ambayo imekuwa mzigo kwa walipa ushuru. 

Hazina inaeleza kuwa mikopo itatumika kugharamia miradi ya maji, usalama wa chakula , afya ya uzazi, uboreshaji wa sekta isiyo rasmi na Biashara Ndogo na za Kati (MSMEs).

Hazina ilikopa Shilingi bilioni 16.7 kutoka kwa  Shirika la maendeleo la kimatifa  ili kuongeza ufikiaji endelevu na usimamizi wa maji ya ardhini katika mipaka ya Pembe ya Afrika.

Serikali pia ilikopa Shilingi bilioni 2.7 kutoka Mizuho Bank Europe NV ambazo zitatumika kwa vifaa vya matibabu vya Turnkey na kandarasi za ukarabati wa vifurushi ili kuboresha vitengo vya uzazi na watoto wachanga .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved