logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mamake Ruto awasili Bomas kufuatilia matangazo ya matokeo ya urais moja kwa moja

Bi Sarah Cheruiyot aliwasili Jumatatu alasiri akiwa ameandamana na wanafamilia wengine.

image
na Radio Jambo

Habari15 August 2022 - 13:35

Muhtasari


•Bi Cheruiyot  amewasili katika ukumbi wa Bomas Of Kenya kabla ya tume ya uchaguzi na mipaka nchini kutangaza matokeo ya urais.

Mamake DP Ruto, Sarah Cheruiyot, wanafamilia wengine katika Bomas Of Kenya

Mamake Naibu Rais William Ruto amewasili katika ukumbi wa Bomas Of Kenya kabla ya tume ya uchaguzi na mipaka nchini kutangaza matokeo ya urais

 Bi Sarah Cheruiyot aliwasili Jumatatu alasiri akiwa ameandamana na wanafamilia wengine. Alikuwa amevalia nguo nyeupe na kofia kichwani alipowasili.

Mama Sarah sasa anaungana na mwanawe Ruto na mkaza mwanawe Rachel Ruto ambao walifika ukumbini mwendo wa saa tisa kasorobo.

Kundi kubwa la wanasiasa na washika dau wengine tayari wamewasili katika ukumbi wa Bomas ili kufuatilia matangazo ya matokeo ya urais.

Chebukati anatarajiwa kumtangaza rais mpya wa Kenya baada ya shughuli ya uhakiki wa fomu za matokeo ya urais kutoka maeneobunge yote na ujumuishaji wa kura  kukamilika.

Uhakiki wa fomu za matokeo ya uchaguzi wa Agosti 9  ulikamilika Jumatatu asubuhi baada ya kuendelezwa kwa siku tano.

Hapo awali, kiongozi wa Roots Party George Wajackoyah na David Mwaure wa Agano walifika katika ukumbi wa Bomas of Kenya kabla ya kutangazwa rasmi kwa matokeo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved