logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbusii afichua wakati alipoanza kukuza rasta zake

Lion pia alitoa maoni yake kuhusu watu kuweka nywele ndefu (rasta).

image
na Radio Jambo

Habari14 November 2022 - 08:14

Muhtasari


• Mbusii alisema  alianza kuzilea mwaka wa 2006 kisha baada ya miaka miwili akanyolewa na maafisa wa usalama.

•Lion alifichua kuwa mtoto wake ambaye anasoma katika shule ya msingi amekuza dreadlocks.

Mtangazaji wa kipindi cha Mbusii na Lion Teke Teke kwenye Radio Jambo Daniel Githinji Mwangi almaarufu Mbusiii amefunguka kuhusu rasta zake.

Katika mahojiano yake na mwandishi Caroline Mbusa, Mbusii alisimulia kinagaubaga kuhusu safari ya kukuza nywele zake ndefu.

Alisema kwamba  alianza kuzilea mwaka wa 2006 kisha baada ya miaka miwili akanyolewa na maafisa wa usalama.

"Serikali walinitandika viboko, wakaziakata zote na panga, nikatulia mwaka mmoja ndipo nikaanza kulea hizi ambazo niko nazo," alisema.

Mtangazaji mwenzake Cyrus Afune almaarufu Lion pia alitoa maoni yake kuhusu watu kuweka nywele ndefu (rasta).

Alieleza kuwa anaunga mkono mtindo huo wa nywele kwani kulingana naye, 'warasta' ni watu ambao wanapenda mambo ya kweli.

"Dreadlocks ni zetu na tuko hapa kuzikubali na kuzithamini. Si lazima kuwa na dreadi ili kuwa rasta," Lion alisema.

Alifichua kuwa mtoto wake ambaye anasoma katika shule ya msingi amekuza dreadlocks baada ya serikali kuukubali mtindo huo wa nywele.

Lion alisema kuwa warasta ni watu wazuri na ni watu wa kawaida, kinyume na wanavyodhani wengine kuwa ni watu wabaya.

"Msiwaone watu wenye dready kama wakora,ama kuwa ni watu wanaovuta bangi. Bangi ni mihadarati ambayo huvutwa hata na watu ambao hawana mtindo huo wa nywele," Mbusii alikubaliana na mwenzake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved