logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mmeona chochote?" Mammito aaibika baada ya zipu ya suruali kuwa wazi akiwa jukwaani

"Poleni jamani. Wah! mmeona. Je, mmeona chochote?," aliwauliza wasikilizaji.

image
na Radio Jambo

Habari25 January 2023 - 12:00

Muhtasari


•Mammito alipatwa na kipindi cha aibu jukwaani wakati wa moja ya shoo za vichekesho siku chache zilizopita.

•"Hiyo ilikuwa aibu. Nini? Ni vizuri umeniambia (Wanda) nimefanya hivyo," alisema.

Mchekeshaji Eunice Mammito alipatwa na kipindi cha aibu jukwaani wakati wa moja ya shoo za vichekesho siku chache zilizopita.

Mamitto alikuwa akitumbuiza kwenye jukwaa wakati mmoja wa wachekeshaji wenzake, Justice Wanda, alipogundua kuwa zipu ya suruali yake ilikuwa chini na akapanda hadi pale  jukwaani kumjulisha mbele ya hadhira yake.

Wanda alionekana akinong'ona maneno yasiyosikika kwenye sikio la mchekeshaji huyo wa Churchill Show ambaye mara moja aliinama kidogo ili kuvuta zipu yake juu huku aibu kubwa ikiwa imeandikwa usoni mwake.

"Poleni jamani. Wah! mmeona. Je, mmeona chochote?," aliwauliza wasikilizaji wake ambao walisikika wakicheka kwa nguvu.

Baadaye  alionekana kufarijika na akajiunga na mashabiki kwa kicheko baada ya kushawishika kuwa hawakuona chochote.

"Hiyo ilikuwa aibu. Nini? Ni vizuri umeniambia (Wanda) nimefanya hivyo," alisema.

Mchekeshaji huyo alitania kwamba wanaume walikuwa wakimtazama sana kwa sababu zipu yake ilikuwa chini.

"Jamani mlifurahi sana. Ndio maana wanaume walikuwa wakinitazama hivyo, nilikuwa najiuliza kuna nini? Nyote hamwezi kuwa mnatabasamu hivyo," alisema.

Zaidi, alifanya utani kwamba alikuwa ametoka kwenye kipindi kifupi cha mapenzi.

Tazama video:-


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved