logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sababu kwa nini Igathe alisusia hafla ya kuapishwa kwa Sakaja

"Nataka kumtambua mshindani wangu Igathe. Nilikaa naye hivi majuzi na alijipa udhuru leo ​​akisema anasafiri" - Sakaja alisema.

image
na

Habari25 August 2022 - 12:26

Muhtasari


• Johnson Sakaja aliapishwa kama gavana wa nne wa Nairobi.

• Sakaja alimshinda Igathe na kuzoa kura 699, 392 huku Igathe akipata kura 573, 516.

Johnson Sakaja akiwa na mkewe wakati wa kuapishwa kwake kama Gavana wa Nairobi mnamo Agosti 25, 2022.

 Johnson Arthur Sakaja sasa ndiye rasmi Gavana mpya wa Nairobi. Aliapishwa katika hafla rasmi iliyofanyika KICC.

Jaji Roselyne Aburili kwa kusaidiwa na hakimu Caroline Kabucho waliwaapisha Sakaja na naibu wake, Njoroge Muchiri.

Mbali na hayo, hakimu pia anasimamia utiaji saini wa hati ya uadilifu kwa wawili hao.

Akizungumza baada ya kuapishwa kwake Sakaja alifichua ni kwa nini mpinzani wake Polycarp Igathe alikosekana kwenye hafla hiyo.

"Nataka kumtambua mshindani wangu Igathe. Nilikaa naye hivi majuzi na alijipa udhuru leo ​​akisema anasafiri. Kugombea madaraka ni kitendo cha uzalendo. Asante Polycarp kwa kusogeza mbele siasa zetu kwa njia chanya zaidi. Wewe ni mfano halisi wa Siasa safi, kitu ambacho ninaamini."

Sakaja aliwashukuru wagombea wengine wote wa ugavana akiongeza kuwa anatumai wanaweza kufanya kazi pamoja.

Alisema alifurahi kuwa kampeni ya 2022 haikuegemea utambulisho wa kibinafsi bali ajenda zinazowaunganisha Wakenya. Aliwashukuru wenyeji wa Nairobi kwa kudumisha amani.

Sakaja hivi majuzi alikutana na Igathe kwa tafrija ya kahawa jambo lililowafanya Wakenya kushangaa. Wengi walidhani ni maadui kutokana na kuwa wanawania kiti kimoja lakini hiyo ni mbali na ukweli.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved