logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wanawake wananipenda, nawapenda pia!" DJ Fatxo azungumzia madai ya kuwa shoga

Alibainisha kwamba hata hajawahi kupatwa na wazo la kuwa mpenzi wa jinsia moja

image
na Radio Jambo

Habari23 May 2023 - 06:50

Muhtasari


•Katika mahojiano, alisema madai  ya ushoga ni uvumi tu ulioanzishwa na kuenezwa na maadui zake ambao hakufichuliwa.

•Mwimbaji huyo wa nyimbo za Kikuyu mwenye umri wa miaka 27 aliweka wazi kuwa anawapenda sana wanawake na wanampenda pia.

Mwimbaji wa Mugithi Lawrence Njuguna almaarufu DJ Fatxo amejitenga mbali na kundi la wapenzi wa jinsi moja almaarufu LGBTQ.

Katika mahojiano na Mpasho, alisema madai  ya ushoga ni uvumi tu ulioanzishwa na kuenezwa na maadui zake ambao hakufichuliwa.

Alibainisha kwamba hata hajawahi kupatwa na wazo la kuwa mpenzi wa jinsia moja

"Sijawahi kuwa, sitawahi kuwa na mimi si wa LGBTQ," Fatxo alisema.

Mwimbaji huyo wa nyimbo za Kikuyu mwenye umri wa miaka 27 aliweka wazi kuwa anawapenda sana wanawake na wanampenda pia.

"Kuhusu kuwa mashoga, wanawake wananipenda na mimi nawapenda. Mimi sio shoga na siwezi," alisema.

Uvumi wa msanii huyo kuwa shoga uliibuka baada ya kuhusishwa na kifo cha Jeff Mwathi ambaye alifariki nyumbani kwake mwezi Februari.

Fatxo alikanusha madai ya kutumia mwanadada anayeaminika kuwa mpenzi wake kuficha kuwa yeye ni shoga huku akieleza mshangao wake kuhusu kwanini wanawake ambao amekuwa nao hawakujitokeza kumtetea.

"Ilikuwa ni jambo chungu zaidi kwangu(kuhusishwa na ushoga) kushinda mambo mengine mnaniwekelea kwa sababu nilitarajia wanadada wote ambao nimekuwa nao watokee waongee wanitetee waseme mimi sio shoga," alisema.

Kufuatia kifo chake, kulikuwa na madai kwamba marehemu Jeff Mwathi huenda alidhulumiwa kimapenzi kabla ya kudaiwa kuuawa, madai ambayo wanapatholojia walijaribu kuchunguza lakini kwa bahati mbaya hawakuweza kupata majibu kwa sababu muda mwingi ulikuwa umepita tangu kifo chake. Sampuli za DNA zilichukuliwa kutoka kwa DJ Fatxo na washirika wake waliokuwa na marehemu kabla ya kifo chake  ili kusaidia uchunguzi huo.

Siku ya Jumatatu, mwimbaji huyo alisisitiza kwamba hakuhusika katika kifo cha kijana huyo ambaye alitambulisha kama rafiki yake.

"Jeff alikuwa rafiki yangu. Sioni sababu yangu kumuua," alisema.

Mamake Jeff Mwathi hata hivyo  alisisitiza kwamba bado anaamini mwimbaji huyo wa Mugithi alihusika.

"Hata yeye anafaa kupitia kitu kama hiyo. Alifanya vibaya sana, kuua mtoto wa mtu hivo hadharani," alisema.

Alilalamika kwamba haki haikutenda kwa mwanawe huku akipuuzilia mbali uchunguzi uliofanyiwa na DCI.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved