logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wazazi wapya mjini! Nadia Mukami na Arrow Bwoy wabarikiwa na mtoto wa kiume

Arrow Bwoy alitaja mwanao kama zawadi nzuri kuwahi pokea maishani.

image
na Radio Jambo

Habari26 March 2022 - 04:19

Muhtasari


•Arrow Bwoy alitaja mwanao kama zawadi nzuri kuwahi pokea maishani.

Wanandoa mashuhuri Nadia Mukami na Arrow Bwoy wamemkaribisha mtoto wao wa kwanza duniani.

Nadia alijifungua mtoto wa kiume mnamo siku ya Alhamisi, Machi 24.

Wakithibitisha habari hizo njema kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii, wawili hao wao walifichua kuwa jina la mwanao Haseeb Kai.

"Karibu katika ulimwengu wetu Haseeb Kai. Machi 24, 2022," Nadia aliandika chini ya picha iliyoonyesha akiwa amelala katika wodi ya uzazi na mumewe kando yake akiwa amemshika mtoto wao mikononi.

Arrow Bwoy alitaja mwanao kama zawadi nzuri kuwahi pokea maishani.

"24.03.2022 tumepokea zawadi nzuri zaidi Haseeb Kai. Karibu kwenye ulimwengu wetu," Arrow Bwoy aliandika.

Wazazi hao wapya tayari wamefungulia mtoto wao ukurasa wa Instagram ambao umeweza  kujizolea wafuasi zaidi ya elfu nne.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved