Mbunge wa Nyeri Mjini Ngunjiri Wambugu jana amewaambia viongozi hao kwamba nafasi ya urais itakuwa wazi mwaka wa 2022 na kwa sasa wanafaa kutekeleza majukumu yao .
“ Tuna rais aliye afisini hadi mwaka wa 2022 , kama tu msiovyoweza kumruhusu mtu kufanya kampeini za kiti change kwani nipo kama mbunge ,pia hapafai kuwa na kampeini za kiti cha urais’ amesema Wambugu .
Mbunge huyo amesema hawapingi wenzake katika chama cha Jubilee lakini anatawaka watii agizo la kinara wa chama Rais Kenyatta kukomesha kampeini za mapema .
Alikuwa akizungumza katika kanisa la Nyamachaki PCEA mjini Nyeri ambapo alisambaza hundi za cheki zenye thamani ya shilingi milioni 27 .2 kwa wanafunzi wa shule za upili na vyuo vikuu katika eneo bunge lake .
