logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond Platnumz awapeleka Zari na watoto wake katika ziara ya jumba lake kubwa

Zari amewaleta watoto Tanzania kumuona baba yao

image
na Radio Jambo

Habari08 November 2020 - 08:03

Muhtasari


  •  Diamond hajawaona watoto wake kwa miaka miwili 
  •  Zari amewaleta watoto Tanzania kumuona baba yao 
  • Wawili hao walitengana  mwaka wa 2018 

 

Zari Hassan Diamond Platnumz  wameendelea kuzima mitandao nchini Tanzania baada ya  Zari kuwaleta watoto wake ili kumuona baba yao  na kila hatua wanayochukua imeteka nyara ndimi za wengi .

 Diamond hajawaona wanawe kwamiaka miwili tangia mwaka wa 2018 wakati alipotengana na Zari  na amekuwa akionyesha matamanio makubwa sana ya kuwaona watoto wake .

View this post on Instagram

Mng......πŸ–

A post shared by Sandrah...! (@mama_dangote) on

 Ziara hiyo imefanyika baada ya Staa huyo kumtaka mpenzi wake wa zamani Zari kuja Tanzania kwa sababu ya shughuli zake nyingi na hangeweza kwenda Afrika Kusini kuwaona wanawe . Zari alitangaza ziara hiyo  kwa kuweka picha wakiwa katika ndege ya Kenya Airways katika kurasa za mitandao ya kijamii za watoto  wake .

 Kulikuwa na shughuli nyingi katika uwanja wa ndege walipotua huku wanagabari wengi wakitaka kuwapiga picha na kuwahoji walipolakiwa na Diamond .

 Diamond  baadaye alionekena akiwapeleka Zari na watoto wake katika kila chumba  cha kasri lake akiwaonyesha pia tuzo nyingi ambazo amejishindia katika fai ya muziki .

 Katikia video nyingine ameonekana akiwachezea gita watoto hao huku Zari akiwa pembeni akiangalia kwa tabasamu . Wengi wanajiuliza iwapo Zari na Diamond wataweka kando fahari yao na kurudiana ingawaje wote wamekanusha hilo

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved