logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Misa ya wafu ya Magufuli: Hisia kali zamzonga mama Janet Magufuli

Misa ya wafu ya Magufuli: Hisia kali za mzonga mama Janet Magufuli

image
na Radio Jambo

Habari22 March 2021 - 08:44

Muhtasari


• Janet ambaye alikuwa ameketi karibu na Rais wa Tanzania Saumu Suluhu alionekana akilia bila kudhibitiwa huku akibubujikwa na machozi.

Mjane wa hayati rais Pombe Magufuli, Janet Magufuli azidiwa na hisia wakati wa misa ya wafu ya mwendake mumuwe.

Mjane wa hayati John pombe Magufuli -Janet Magufuli siku ya Jumatatu alizidiwa na hisia wakati mwili wa mumuwe ulifika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kwa mazishi ya serikali.

Janet ambaye alikuwa ameketi karibu na Rais wa Tanzania Saumu Suluhu alionekana akilia bila kudhibitiwa huku akibubujikwa na machozi.

Janet, aliyevaa nguo nyeusi, alionekana akifarijiwa kwenye jukwaa kuu hata wakati mwili wa mumewe ulipowasili.

Umati uliposimama kuupokea mwili, Janet hakuweza kuhimili akalia hata zaidi huku akifuta machozi yake kwa leso jeupe.

Alibaki ameketi wakati wa wimbo wa Afrika Mashariki ulipokuwa ukichezwa.

Rais Suluhu alionekana akinyoosha mkono wake kuelekea kwa Janet alipojaribu kumfariji bila mafanikio.

Wanawake wawili ambao walikuwa kando ya Janet wakijaribu kumfariji pia walionekana wakijaribu kuzuia machozi.

Rais Uhuru Kenyatta ni miongoni mwa viongozi wa nchi ambao wako Dodoma kwenye Uwanja wa Jamhuri kwa misa ya wafu ya ya Magufuli.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved