logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya yapokea chanjo zaidi za AstraZeneca

Kenya yapokea chanjo zaidi za AstraZeneca

image
na Radio Jambo

Habari21 May 2021 - 04:56

Muhtasari


• Mkuu wa kikosi kazi cha utoaji wa chanjo za Covid-19 Dkt Willis Akhwale alithibitisha kuwa dozi hizo zilifika salama mjini Nairobi siku ya Alhamisi.

• Wakenya wanapaswa kutarajia kupokea chanjo ya pili kuanzia mapema wiki ijayo.

• Akhwale alisema wataanza na Wakenya ambao walipokea dozi ya kwanza mwezi Machi kwa sababu wanahitaji kupewa ya pili ndani ya kipindi cha wiki 12.

Kenya imepokea zaidi ya dozi 130,000 za chanjo ya AstraZeneca Covid-19.

Chanjo hizo, ambazo zilifika Nairobi siku ya Alhamisi asubuhi, zilitoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambayo ilisema haikuwa na uwezo wa kutoa dozi milioni 1.3 kabla ya kumalizika kwa muda wa matumizi Juni 24.

DRC ilipokea dozi milioni 1.7 kupitia Covax mnamo Machi 2 lakini imetumia tu chanjo 400,000 baada ya kuzuka kwa hofu kuwa chanjo hiyo inaweza kusababisha kuganda kwa damu.

Unicef ​​iligawanya dozi zilizobaki kwa nchi kadhaa ikiwa ni pamoja na Kenya, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ghana, Senegal na Togo.

Mkuu wa kikosi kazi cha utoaji wa chanjo za Covid-19 Dkt Willis Akhwale alithibitisha kuwa dozi hizo zilifika salama mjini Nairobi.

Alisema dozi zingine 136,000 zilibaki kutoka kwa zoezi la kwanza la chanjo nchini Kenya.

Jumla ya dozi 266,000 sasa zitapewa Wakenya ambao walipokea dozi ya kwanza mnamo mwezi Machi.

“Wakenya wanapaswa kutarajia kupokea chanjo ya pili kuanzia mapema wiki ijayo. Tutaanza na Wakenya ambao walipokea dozi ya kwanza mwezi Machi kwa sababu wanahitaji kupewa ndani ya kipindi cha wiki 12, ”Akhwale alisema.

Hii inamaanisha kuwa Kenya imewapa chanjo karibu watu 950,000 tangu zoezi hilo lilipoanza Machi 5.

Kenya ilipokea dozi milioni 1.02 za chanjo ya AstraZeneca-Oxford kutoka Covax mnamo Machi 3, na msaada wa dozi 100,000 kutoka kwa serikali ya India Machi 11.

Dkt. Akhwale alisema kwamba Kenya pia itapokea karibu dozi milioni mbili za chanjo ya Johnson & Johnson mwezi Agosti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved