logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aston Villa yatangaza usajili wa Emiliano Buendia kutoka Norwich

Klabu ya Arsenal ilikuwa inamumezea mate kiungo huyo kwa muda ila zabuni ya Aston Villa ikakubalika kwani ilipiku ile ya Arsenal.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri07 June 2021 - 09:53

Muhtasari


•Klabu ya Norwich imetangaza kuwa uhamisho wa Buendia ndio mkubwa zaidi kuwahi fanyika katika klabu hiyo.

•Habari zingine kuhusiana na uhamisho huo zitatolewa baada ya vipimo vya kidaktari kukamilika.

Emiliano Buendia baada ya kushinda kombe la Championship na klabu ya Norwich

Klabu ya Aston Villa imetangaza usajili wa kiungo matata Emiliano Buendia kutoka klabu ya Norwich City.

Kupitia mtandao wa Twitter, klabu hiyo ambayo ilimaliza katika nafasi ya 11 kwenye ligi kuu Uingereza imesema kuwa imefikia makubaliano na klabu ya Norwich kumchukua kiungo huyo.

Huku Emiliano akiwa nchini Argentina kwenye matayarisho ya mchuano wa kuhitimu kucheza Kombe la Dunia dhidi ya nchi ya Kolombia siku ya Jumanne, anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya kidaktari baada ya mechi hiyo” Klabu ya Aston Villa ilitangaza.

Klabu ya Arsenal ilikuwa inamuwinda kiungo huyo kwa muda  pia  ila zabuni ya Aston Villa ikapiku ile ya Arsenal na kwa hivyo kukubalika.

Klabu ya Norwich imetangaza kuwa uhamisho wa Buendia ndio mkubwa zaidi kuwahi fanyika katika klabu hiyo.

Kulingana na ripoti mbali mbali za kitaifa, iligharimu klabu ya Aston Villa takriban poundi milioni 34 na maongezi  mengine juu yake kumfanya Buendia kuwa mchezaji ghali zaidi kuwahi uzwa na klabu ya Norwich.

Habari zingine kuhusiana na uhamisho huo zitatolewa baada ya vipimo vya kidaktari kukamilika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved