logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ulikuwa wakati wangu wa kuondoka,hakuhusiani na Raila-Sossion

Hii ni mara ya kwanza kwa bosi wa zamani wa Knut kuzungumza baada ya kutangaza kujiuzulu

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 July 2021 - 11:00

Muhtasari


  • Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Kitaifa wa Walimu nchini Kenya Wilson Sossion amekanusha madai kwamba alijiuzulu  baada ya kushawishiwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga
Katibu Mkuu wa Muungano wa KNUT Wilson Sossion

Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Kitaifa wa Walimu nchini Kenya Wilson Sossion amekanusha madai kwamba alijiuzulu kutoka kwa umoja huo baada ya kushawishiwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga.

Akizungumza Jumatatu jioni, Sossion alisema kwamba bosi wa chama cha Orange anaheshimu demokrasia, akisisitiza kwamba alijiuzulu kutoka Knut kwa mapenzi yake mwenyewe.

"Hio ni porojo. Raila hawezi na anaheshimu demokrasia ya watu, kwa hivyo hiyo ni fitina… Ilikuwa hiari yangu mwenyewe," Sossion alisema akiwa kwenye runinga moja humu nchini.

Mbunge mteulliwa alibaini kuwa Raila ni kiongozi wa chama chake na wakati wowote wanapokuwa na mazungumzo; kawaida ni kuhusu siasa na mambo ya wafanyikazi wa Kenya bungeni.

"Nimeshinikiza nyongeza ya mishahara kwa walimu, nimeshinikiza kuajiriwa kwa walimu na nikaona kuwa nimetimiza mengi katika umoja lakini ulikuwa wakati wa mimi kuondoka," aliongeza.

Hii ni mara ya kwanza kwa bosi wa zamani wa Knut kuzungumza baada ya kutangaza kujiuzulu kutoka kwa chama cha walimu.

Sossion alijiuzulu mnamo Juni 25, baada ya miaka mitatu ya mzozo wa uongozi katika umoja na Tume ya Huduma ya Walimu.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved