logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wakati wa siasa chafu umwekwisha!' Mudavadi akosoa wanasiasa wanaohadaa Wakenya kwa kuwapa hongo

Mudavadi amesisitiza kuwa ufufuaji wa uchumi na kubuni ajira kwa vijana ndilo lengo lake kuu

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 July 2021 - 04:30

Muhtasari


• Musalia Mudavadi amewataka wakenya kuweka kwenye mizani sera na agenda zitakazokuwa zikipigiwa uungwaji mkono na wagombeaji mbali mbali wa nyadhifa za uongozi wa kisiasa kwenye kura ya mwaka 2022.

•Amepuuzilia mbali siasa za mrengo wa upinzani wa NASA na kusema kuwa Imani ya wafuasi wa NASA imedidimia pakubwa na kwake anasaka kufufua Imani hiyo na mwanzo mpya. 

Kinara wa ANC Musalia Mudavadi. Picha:HISANI

Kinara wa chama cha ANC Musalia Mudavadi amewataka wakenya kuweka kwenye mizani sera na agenda zitakazokuwa zikipigiwa uungwaji mkono na wagombeaji mbali mbali wa nyadhifa za uongozi wa kisiasa kwenye kura ya mwaka 2022.

Akiwa Nyeri alipomtembelea Gavana wa Kaunti ya Nyeri Mutahi Kahiga Mudavadi amesisitiza kuwa ufufuaji wa uchumi na kubuni ajira kwa vijana ndilo lengo lake kuu kwenye kusaka kura za wakenya za Urais ifikiapo debe la mwaka 2022.

Amewakososa viongozi wanaowahadaa wananchi na hasa vijana kwa kuwapa hongo na kiinua mgongo huku wakidai kuwa wao ndio watakaofufua uchumi wa taifa la Kenya.

Mudavadi akisema kuwa wakati wa siasa chafu umekwisha na sasa ni sharti wakenya wazinduke na kufahamu kuwa sera bora ndizo ambazo zitalikomboa taifa hili.

Mudavadi alitumia fursa hii kutilia shime suala la uaminifu kwenye miungano na kusema kuwa chama cha ANC kinasaka marafiki waaminifu ambao wataketi kwenye meza ya mazungumzo na yale watakayoafikiana yasiwe tu kwenye wino wa karatasi bali yawe yale watakayoyatenda kwa vitendo kwa minajili ya kuwapa wakenya mwamko mpya.

Amepuuzilia mbali siasa za mrengo wa upinzani wa NASA na kusema kuwa Imani ya wafuasi wa NASA imedidimia pakubwa na kwake anasaka kufufua Imani hiyo na mwanzo mpya.

Baadaye alikutana na wadau mbali mbali na kusemezana nao ana kwa ana na Hapo kesho atahudhuria Ibaada kadhaa za jumapili Nyeri na pia kukutana na wananchi wa tabaka mbali mbali ili kukuza azma ya safari yake ya Ikulu.

Alikuwa amaendamana na viongozi kadhaa wa ANC kutoka mlima Kenya Pamoja na wabunge Sakwa Bunyasi na Beatrice Adagala na Mwenyekiti wa ANC Kelvin Lunani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved