logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kanze Dena asema Uhuru hatamaliza miradi ya ajenda 4

Kanze Dena amesema rais Kenyatta hatafanikiwa kumaliza miradi ya ajenda nne kuu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 March 2022 - 07:48

Muhtasari


• Msemaji wa ikulu Kanze Dena amesema kwamba rais Uhuru Kenyatta hatafanikiwa kumaliza miradi yote ya ajenda nne kuu mwezi Agosti ambapo atakuwa anakamilisha kipindi chake cha uongozi.

• “Kuna miradi ya ujenzi wa nyumba inayoendelea kule Mtwapa na Buxton, miongoni mwa maeneo mengine,” alisema.

State House/ Twitter

Msemaji wa ikulu Kanze Dena amesema kwamba rais Uhuru Kenyatta hatafanikiwa kumaliza miradi yote ya ajenda nne kuu mwezi Agosti ambapo atakuwa anakamilisha kipindi chake cha uongozi.

Akifanya mahojiano na kituo kimoja cha habari nchini Jumanne, Kanze alisema kwamba baadhi ya miradi ipo ndani ya ruwaza ya 2030 na itakamilishwa na serikali inayofuata.

“Hata hivyo,serikali hii ya Jubilee imepiga hatua kubwa sana katika mpango wa ajenda nne kuu ikiwemo katika miradi ya uzalishaji, upatikanaji wa chakula miongoni mwa mingine,” Kanze alisema.

 Kulingana naye, japo miradi mingi inaendelea kushughulikiwa, kumeshuhudiwa ufanisi mkubwa katika utekelezwaji wa miradi hiyo.

“Kuna miradi ya ujenzi wa nyumba inayoendelea kule Mtwapa na Buxton, miongoni mwa maeneo mengine,” alisema.

Aliongezea kwamba handshake kati ya rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga ilisaidia kumaliza miradi mingi zaidi.

Kanze alisema kwamba rais Kenyatta anashirikiana na kaunti za eneo la Pwani ili kutoa hatimiliki 500,000 kwa wakazi wa eneo hilo.

Pia aliwataka wakazi kutafuta mbinu mbadala za kuzalisha chakula ili kutatua zogo la ukosefu wa chakula hasahasa katika vipindi vya kiangazi.

Alisema kuwa kufufuliwa kwa bandari ya Liwatoni kumechangia pakubwa ufanisi wa biashara ya bahari.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved