logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mwambieni awache kinipa block,'Harmonize asema baada ya kununulia Kajala mkufu wa milioni 5

Anadhani kuwa Kajala ndiye suluhisho pekee.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 April 2022 - 14:18

Muhtasari


  • Harmonize alinunua cheni hiyo kwa Tsh 5Milioni, na akasema ni ya aliyekuwa mpenzi wake Kajala na ana uhakika Kajala atamrudia
Harmonize na Frida Kajala

Hakika Harmonize yuko kwenye mapenzi na anajaribu kufanya kila linalowezekana ili Kajala amrudie tena.

Baada ya kuomba mitandaoni na hata kuweka bango kwenye moja ya barabara za Tanzania, na bado hajapata majibu kutoka kwa ex wake Kajala, Harmonize ameamua kutumia pesa nyingi zaidi.

Leo tarehe 6 Aprili 2022, Harmonize alienda kwenye duka la vito na akatambua cheni ya dhahabu ambayo Kajala alikuwa akiipenda sana.

Harmonize alinunua cheni hiyo kwa Tsh 5Milioni, na akasema ni ya aliyekuwa mpenzi wake Kajala na ana uhakika Kajala atamrudia.

Harmonize anatumai kuwa Kajala atarejea kama inavyofahamika Harmonize amekuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi tofauti baada ya kuachana na Kajala lakini mambo hayakumwendea vyema.

Anadhani kuwa Kajala ndiye suluhisho pekee.

Pia msanii huyo aliwasihi wanamitandao kushauri Kajala awache kumpa block kwenye mitandao ya kijamii.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved