logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watoto wa Mitaani wabadilisha Mbwa kitoweo-Molo

watoto hao hawajawahi kulazwa

image
na

Makala24 June 2022 - 09:43

Muhtasari


•Wakaazi hao wa Molo wameiomba serikali kubuni mpango utakaosaidia wavulana wa mitaani kupata chakula na malazi.

•Baadhi ya sababu ya watoto hawa kujiingiza kwenye vitendo hivyo ni kutokana na ukosefu wa kazi, na njaa ambayo imeikumba nchi.

Mbwa waliofungiwa kwa ajili ya kuchinjwa huko Korea

Watoto wa mitaani huko Molo wamechinja Mbwa na kuibadilisha kuwa kitoweo,tukio hilo ilidhibitishwa na mkaaji  wa Molo Simon Munene akizungumza na wanahabari.

''Niliona moshi kutoka kwenye nyumba,nikadhani  kuwa inaungua,kufika ndani nikakuta nyama sakafuni kiko tayari  kupikwa'' Simon alisema.

Wavulana hao walisema kuwa  walihisi njaa na hii iliwalazimu kuchinja mbwa iliwapate kitu cha kukula.

Wakaazi hao wa Molo wameiomba serikali kubuni mpango utakaosaidia wavulana wa mitaani kupata chakula na malazi.

''Najua maisha ni magumu, lakini hapa Molo hatujafikia kiwango hicho cha kula mbwa, hawa watoto wa mitaani wanateseka kwa kweli'' Simon alisema.

Wakaazi wa Molo pia wamekubali kukuja na mpango ambao utawasaidia watoto wa mitaani kupata vyakula na malazi.

Mchango mdogo kutoka kwa wakaazi hao ili kutimiza ndoto hii ni kitu ambacho kimeungwa mkono na watu wengi.

''Ninajua ya kwamba wale ambao watafikiwa na jambo hili,tushirikiane pamoja ili kusaidia hawa watoto,kama uko na Viazi, chochote kile wewe leta''Simon alisema.

Aliongeza kwa kusema kuwa Chifu, Mwakilishi Wadi na Mbunge  wa eneo hilo wajitokeze wote kuwasaidia watoto hawa,kuna wengine wanahitaji kupelekwa Hospitalini.

''Mpango huu utasaidia hawa watoto kwa kupata mahitaji ya msingi katika maisha ya mwanadamu'' aliongezea.

Baadhi ya sababu ya watoto hawa kujiingiza kwenye vitendo hizo ni kutokana na ukosefu wa kazi, na njaa ambayo imekumba nchi.

Pia iliripotiwa kuwa watoto hao hawajawahi kulazwa hospitalini kwa shida yoyote inayotokana na kukula  Mbwa,Paka, Panya na Punda kwa zaidi ya miaka miwili.

''Punda anapogongwa na gari wanalikusanya kisha wanalipika, jambo la kusikitisha ni kwamba, wakikutwa na Polisi wakiwa wamelala nje , wanakamatwa na kupelekwa selI badala ya serikali kuwasaidia  kupata kazi na chakula'' John alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved