logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa mkuu wa mauaji ya kiholela Nakuru akamatwa

Polisi wamegundua kuwa mshukiwa si mageni kwa jela na ana historia ya uhalifu.

image
na

Yanayojiri01 July 2022 - 06:25

Muhtasari


• Imethibitishwa mauaji yote yaliyolenga wanawake na yalifanywa wakati wa mchana, na miili ya wahasiriwa kupatikana katika chumba cha kulala.

Polisi wamemkamata mshukiwa mkuu wa mauaji ya kiholela ambayo yametikisa eneo la Mawanga, Nakuru kaskazini siku za hivi majuzi.

Evans Michori Kebwaro, alifuatwa hadi maficho yake Alhamisi alasiri eneo la Keroka, Kaunti ya Kisii, alikokuwa amejificha mara baada ya maafisa wa upelelezi kuanzisha msako.

Baadaye aliwafichua washirika wake watano Julius Otieno, 27, Josphat Simiyu, 24, Dennis Mmbolo 25, Isaac Kinyanjui, 18 na Makhoha Wanjala, 25, ambao wote wamejumuishwa katika operesheni ya siri iliyoendeshwa Nakuru, na kikosi maalum cha maafisa wa upelelezi.

Polisi wamegundua kuwa mshukiwa si mageni kwa maisha ya jela na ana historia ya uhalifu, ambayo hapo awali alipatikana na hatia na alitumikia vifungo gerezani.

Haya yanajiri baada ya mkutano wa hadhi ya juu wa usalama ambao ulifanyika mjini Nakuru ukiongozwa na waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang’i, kufuatia agizo la rais.

Imethibitishwa mauaji yote yaliyolenga wanawake na yalifanywa wakati wa mchana, na miili ya wahasiriwa kupatikana katika chumba cha kulala baada ya kuchomwa moto. Washukiwa hao waliletwa Nairobi kwa uchunguzi zaidi na maafisa wa DCI.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved