logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sijazungumza na Uhuru kwa miezi kadhaa lakini nitampigia simu hivi karibuni - Ruto

"Nitampigia simu Rais Uhuru Kenyatta," Ruto alisema.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 September 2022 - 16:12

Muhtasari


  • “Hatuna suala na uchaguzi wa kidemokrasia wa Wakenya. Nilipomuunga mkono sikumpa sharti la kuniunga mkono,” alisema

Rais mteule William Ruto amefichua kwamba hajazungumza na Rais Uhuru Kenyatta kwa miezi mingi.

Haya yanajiri licha ya kwamba alitangazwa kuwa Rais mteule na IEBC mnamo Agosti 15. Inatarajiwa kuwa rais aliyeko madarakani angemshirikisha katika masuala ya mpito.

Katika hotuba yake ya kwanza kwa taifa baada ya Mahakama ya Juu kuidhinisha ushindi wake, Ruto alisema atawasiliana na Rais anayeondoka baada ya hotuba yake kujadili mbinu za mpito.

"Nitampigia simu Rais Uhuru Kenyatta," Ruto alisema.

"Hatujazungumza kwa miezi lakini hivi karibuni nitapiga simu ili tufanye mazungumzo juu ya mchakato wa mpito."

Ruto alisema Uhuru alifanya kazi kwa bidii kwa njia zake mwenyewe katika kumuunga mkono mgombeaji wake kipenzi Raila Odinga lakini akabainisha kuwa Wakenya walifanya uamuzi wao.

“Hatuna suala na uchaguzi wa kidemokrasia wa Wakenya. Nilipomuunga mkono sikumpa sharti la kuniunga mkono,” alisema.

"Tutabaki, marafiki, kama tumekuwa katika muktadha wa tulipo na tunatarajia kujenga msingi uliopo."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved