Je, unajua kuwa sasa zimesalia siku 16 pekee kusajili simcard yako ya Safaricom? Tarehe ya mwisho ya Oktoba 15 iliyowekwa na Mamlaka ya Mawasiliano inakaribia na namba yoyote ya simu ambayo maelezo yake hayajaunganishwa moja kwa moja na mtu anayeweza kutambuliwa itazimwa.
Hii inamaanisha kuwa ikiwa laini yako ya Safaricom itazimwa hutaweza kupiga simu, hutaweza kutumia Mpesa (iwe kwa matumizi ya kibinafsi au ya biashara) na pia hutaweza kutumia mtandao.
Zoezi la usajili wa laini hukuruhusu kuthibitisha namba zote za simu zilizosajiliwa chini ya kitambulisho chako ili kuepuka usajili mara mbili na hatari ya ulaghai.
Usipoteze nafasi yako ya pili ya kujiandikisha kwani hii ndiyo nafasi ya mwisho ya kufanya hivyo kulingana na kanuni za serikali.
Safaricom imewezesha mchakato wa usajili wa kidijitali na unaweza kutekeleza zoezi hili mtandaoni peke yako ukiwa nyumbani kwako.
Kuna njia tofauti unaweza kusasisha na kuthibitisha maelezo ya Simcard yako:
- Ili kuthibitisha stakabadhi zako za usajili wa laini, bofya link hii https://safaricom.com/account/kyc-upload na ufuate hatua rahisi. Utahitajika kupakia kitambulisho chako rasmi ulichotumia wakati wa usajili.
- Tumia MySafaricom App: Angalia maelezo ya usajili wa simcard yako kwenye programu ya MySafaricom.
- Zuri: Hifadhi namba 0722 000100 kwenye simu yako, fungua ukurasa wa mazungumzo kwenye WhatsApp na uandike ‘Hi Zuri’ SIM Registration Update.
- Tembelea maduka yoyote ya Safaricom kote nchini. Maajenti wa Safaricom watakagua kitambulisho chako dukani.
- Unaweza pia kutumia chaguo la USSD kwa kupiga *106# na uchague chaguo namba moja ili kuangalia hali yako ya Usajili au chaguo namba mbili kwa sasisho la usajili wa sim.
Usikose tarehe ya mwisho. Linda laini yako ya Safaricom leo!