logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mzee wa miaka 71 afariki kwenye loji akiwa na kidosho wa miaka 22

"Marehemu alianza kulalamika kwa maumivu ya kifua, mgongo na miguu na mikono kufa ganzi"

image
na Radio Jambo

Makala28 January 2023 - 07:50

Muhtasari


• Teksi iliitwa ili kumkimbiza hospitalini lakini akatangazwa kufa walipomfikisha kwenye kituo cha afya.

crime scene

Mwanamume mwenye umri wa miaka 71, ameripotiwa kufariki akiwa na msichana wa miaka 22 katika chumba cha kukodi cha wageni maarufu Guesthouse au ukipenda lodging kwa lugha ya kimombo.

Mzee huyo aliripotiwa kukodi chumba kwa muda mfupi akiwa na kidosho mbichi mwenye umri wa miaka 22 ambaye alimchukua kutoka eneo la Githurai viungani mwa mji wa Nairobi.

Wawili hao baada ya kuingia chumbani, walianza shughuli zao hadi pale msimba ulipotolea katika kile wengi wanahisi kuwa huenda mzee alizidiwa na mbio za langalanga za kidosho huyo.

 "Marehemu alianza kulalamika kwa maumivu ya kifua, mgongo na miguu na mikono kufa ganzi," polisi walisema katika ripoti yao kama ilivyonukuliwa na jarida moja la humu nchini.

Hapo ndipo mwanamke huyo aliposimamisha teksi kumpeleka mzee hospitali.

Kwa mujibu wa polisi dereva wa teksi, ambaye anafahamika sana na mwanamke huyo, alisaidia kumpeleka mzee huyo katika hospitali ya Aga Khan ambapo alitangaza kuwa amefariki alipofika.

Baada ya hapo ndugu wa marehemu aliarifiwa kuhusu kifo hicho.

Polisi walisema mwili huo haukuwa na majeraha yoyote ya kimwili hata kama wapelelezi walianza uchunguzi wa tukio hilo.

Tangu wakati huo wapelelezi wametembelea chumba hicho cha kulala wageni ambapo waliwahoji baadhi ya wafanyakazi waliokuwa zamu wakati wanandoa hao walipopanga chumba chao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved