logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Sina maoni!" Mrembo mpya wa Harmonize ajibu kwa utani kuhusu kuzawadiwa Range Rover

Sishkiki alisema Harmonize ni rafiki wake tu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 March 2023 - 06:30

Muhtasari


• Mrembo huyo alisemwa kuwa mbadala wa Kajala Masanja katika maisha ya Harmonize baada ya kumpakia msanii huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Sishkiki amtaja aliyemnunulia Range Rover.

Mjasiriamali wa kuuza nguo Sishkiki Sikamatiki kutoka nchini Tanzania, mrembo ambaye wiki mbili zilizopita alisemekana kuwa mpenzi mpya wa msanii Harmonize hatimaye amezungumza.

Siku moja iliyopita, mwanadada huyo kwa mara nyingine tena aligonga vichwa vya habari za wambea baada ya gari jipya aina ya Range Rover kuonekana nje ya duka lake la nguo likiwa na jina lake kwenye sehemu ya namba za usajili.

Wengi waling’aka kwamba gari hilo li zawadi ambayo amekabidhiwa kutoka kwa msanii Harmonize, jambo ambalo hata hivyo alisita kulizungumzia huku akikataa katakata kuliweka wazi jina au maelezo ya aliyempa.

Hata hivyo, alikiri kwamba gari hilo ni zawadi aliyokabidhiwa na “mtu anayemdhamini sana” na kusisitiza kwamba hakuna kinachoendelea na Harmonize Zaidi ya urafiki tu.

“Harmonize ni mshikaji wangu, mwanangu kabisa. Tunajuana muda mrefu, ni mtu mzuri sana. Sitaki kuchokonolewa na lile Range Rover nilipewa na mtu anayenidhamini sana. Ila hapo kwa ni nani, sina maoni,” Sishkiki alisema.

Mrembo huyo alisemwa kuwa mbadala wa Kajala Masanja katika maisha ya Harmonize baada ya kumpakia msanii huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram akimtakia kheri njema ya siku yake ya kuzaliwa wiki mbili zilizopita.

Sishkiki alimwandikia Harmonize ujumbe mzuri na kumalizia kwamba anatumai msanii huyo hayuko singo tena kwani yeye yuko.

Hata hivyo, Harmonize naye katika chapisho hilo aliwafanya wengi kukodoa Zaidi macho baada ya kusema kwamba mrembo huyo ni hatari na kumkaribisha katika maisha yake.

Ubadilishanaji wa jumbe hizo uliwafanya wengi kuwa na uhakika usiomithilika kuwa ni wapenzi, mpaka juzi kati za ndani zikaibuka kwamba mfuko wa Harmonize umehusika katika gari hilo lenye hadhi ya nyota tano.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved