logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Azimio kuendelea na maandamano baada ya Ramadhan

Raila alisitisha maandamano baada ya wito kutoka kwa baadhi ya maaskofu na viongozi wenzake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri13 April 2023 - 13:48

Muhtasari


  • Akizungumza Alhamisi wakati wa bazara ya umma, Raila alikiri kuwa Rais William Ruto hakujitolea katika mazungumzo hayo.
Kinara wa Azimio aapa kuendelea na maandamano Jumatatu.

Kiongozi wa Azimio Raila Odinga amesema wanafikiria kufanya maandamano huku mazungumzo yakiendelea.

Akizungumza Alhamisi wakati wa bazara ya umma, Raila alikiri kuwa Rais William Ruto hakujitolea katika mazungumzo hayo.

Alikuwa akijibu wito wa baadhi ya viongozi, wafuasi na washikadau wakati wa kongamano hilo kwamba maandamano hayo yaendelee.

“Mazumgumzo iendelee na maandamano sambamba...dawa ya moto ni moto, kwa hivyo tunaendelea,” alisema Raila.

Alisema atatangaza hatua inayofuata baada ya mwisho wa Ramadhani.

Raila alisitisha maandamano baada ya wito kutoka kwa baadhi ya maaskofu na viongozi wenzake.

Ramadhan inaisha Aprili 21.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved