logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waombolezaji 6 wahofiwa kufariki katika ajali ya Kendu Bay

Basi la Shule ya Sekondari ya ACK Guu lilikuwa likiwasafirisha waombolezaji kuelekea mazishi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri05 May 2023 - 09:22

Muhtasari


•Basi la Shule ya Sekondari ya ACK Guu lilikuwa likiwasafirisha waombolezaji kuelekea mazishi katika wadi ya Karachuonyo Magharibi.

•Shahidi Kenneth Abila alisema lori hilo lilikuwa limetoka barabara ya Kanyadhiang -Pala.

lililohusika katika ajali ya barabarani Mei 5, 2023.

Takriban watu sita wanahofiwa kufariki baada ya basi walimokuwa wakisafiria kuhusika katika ajali ya barabarani karibu na Kanyadhiang, eneo bunge la Karachuonyo.

Ajali hiyo ya Ijumaa ilitokea wakati basi la Shule ya Sekondari ya ACK Guu lilikuwa likiwasafirisha waombolezaji kuelekea mazishi katika wadi ya Karachuonyo Magharibi.

Basi hilo lilipinduka wakati dereva akijaribu kukwepa kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa likija na mwendo kasi.

Wakaazi walisema dereva alipoteza udhibiti wa basi hilo alipokuwa akikwepa lori katika makutano ya Kanyadhiang. Ajali ilitokea kando ya barabara ya Kanyadhiang-Pala wakati basi hilo lilikuwa likipitia kona kutoka barabara ya Kendu Bay -Homa Bay.

Shahidi Kenneth Abila alisema lori hilo lilikuwa limetoka barabara ya Kanyadhiang -Pala.

“Baadhi ya waombolezaji pia wamejeruhiwa na kukimbizwa hospitalini... Lori lilikuwa likienda kwa kasi," Abila alisema.

Kamanda wa polisi wa Kaunti Ndogo ya Rachuonyo Kaskazini Lydia Parteyie alithibitisha kisa hicho akisema basi hilo liliondoka barabarani kabla ya kutua kwenye mtaro.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved