logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilifumania babangu na mke wangu wakifanya mapenzi, sasa wanatarajia mapacha!

Watoto wa Stephanie watakuwa kaka au dada wa kambo wa Declan, ambaye alikuwa mume wake.

image
na Radio Jambo

Makala30 May 2023 - 08:42

Muhtasari


• Darren - ambaye alikataa kutoa maoni - atakuwa babu na baba wa kambo wa Willow ikiwa ataoa Stephanie.

• Watoto wa Stephanie watakuwa kaka au dada wa kambo wa Declan na kaka au dada wa kambo wa Willow na pia shangazi au mjomba wake.

 

Mwanamume mwenye huzuni na mfadhaiko.

Mfanyikazi wa mochwari anasema alitengana na mkewe baada ya kumkamata akishiriki mapenzi na babake - na wanandoa hao sasa wanatarajia mapacha.

Kwa mujibu jarida la The Sun, Declan Fuller, kutoka Rhondda huko South Wales, anadai kuwa alimwona ex wake, Stephanie, pia 22, akiingia chumbani na baba yake mwenye umri wa miaka 44, Darren.

Alipomuuliza Stephanie kilichotokea alisema: 'Tulikuwa tunatazama The Simpsons kwenye TV.'

Darren na Stephanie - ambaye sasa ni mjamzito - wanaishi pamoja karibu maili sita mbali na nyumba ya aliyekuwa mume wake, Fuller.

Lakini Stephanie anasisitiza kuwa hakuwa mwaminifu kwa mpenzi wake wa zamani, akiambia The Sun: 'Sikumsaliti Declan. Tulikutana wiki moja au zaidi baada ya kuniacha.'

Declan alisema: 'Ni kama njama. Sio kawaida. Ninahisi kusalitiwa lakini niko vizuri zaidi bila wao wawili.'

Mume huyo mchanga alitilia shaka baada ya Darren, ambaye ametalikiana, kuhamia naye, Stephanie na binti yao Willow mwenye umri wa miaka miwili Septemba iliyopita.

Miezi miwili baadaye aliangalia kifaa cha kufuatilia mtoto, ambacho alikuwa amebandikiza kwenye mlango wa baba yake.

Watoto wa Stephanie watakuwa kaka au dada wa kambo wa Declan na kaka au dada wa kambo wa Willow na pia shangazi au mjomba wake.

Darren - ambaye alikataa kutoa maoni - atakuwa babu na baba wa kambo wa Willow ikiwa ataoa Stephanie.

Katika taarifa zinazoambatana na hizo, Jumatatu Radio Jambo ilisimulia tukio moja ambalo lilijiri kwenye nyumba ya wageni ambapo mwanamume alikwenda kwenye loji hiyo akiwa na mpango wake wa kando na kumfumania mke wake akitoka na mwanamume mwingine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved