logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hatuachani ni mapunziko tu ya muda- Sauti Sol

Polycarp Otieno amesema kuwa kundi hilo halijatengana ila litachukuwa tu mapunziko ya muda.

image
na

Makala09 June 2023 - 11:16

Muhtasari


• Tamasha hilo la Stanbic Yetu Festival huenda ni mara ya mwisho ambapo mashabiki wa bendi hiyo kuwaona wakitumbuiza pamoja.

• Tamasha hilo ambalo linaandaliwa kwa mara ya pili linafadhiliwa na benki ya Stanbic kwa ushirikiano na kampuni ya Radio Africa Group.

Bendi ya sauti sol.

Mwanachama wa bendi ya Sauti Sol, Polycarp Otieno amesema kuwa kundi hilo halijatengana ila litachukuwa tu mapunziko ya muda.

Akizungumza na vyombo vya habari kabla ya tamasha la Stanbic Yetu Festival, Polycarp alipuuzilia mbali madai ya kuwa kundi hilo litagwanyika kabisa. 

"Imekua safari ya kufurahisha ya miaka 15 kwenye muziki na sasa imefika wakati ambao tunahisi tunafaa kupumzika kwa muda " alisema Polycarp.

Aliwahakikishia mashabiki wao kuwa kundi hilo haliwachi kufanya muziki au kugawanyika ni mapumziko tu ya muda.

"Hatuachi kufanya muziki ama kuachana, ninataka mfahamu hivyo, ni mapunziko tu madogo hakuna kitu kingine", Polycarp alisema.

Aliongeza kuwa..."Imekua safari ya kusisimua ya miaka 15 kwenye muziki pamoja na sasa umefika wakati ambao tunahisi tunafaa kupumzika kwa muda ".

Washindi hao wa tuzo ya MTV kama kundi bora la Afrika mwaka wa 2014 na 2015 walitangaza kuchukua muda wa mapumziko kila mmoja akifanya muziki kivyake. 

Tamasha hilo la Stanbic Yetu Festival huenda ikawa mara ya mwisho ambapo mashabiki wa bendi hiyo watawaona wakitumbuiza pamoja.

Kundi la Boyz II Men walisema pia wao wamewai kuchukua mapunziko kama hio hio inayochukuliwa na kundi hilo la Sauti Sol kwa kipindi cha miaka miwili na iliwaisidia katika taaluma yao ya muziki.

Bendi ya Sauti Sol ni moja wapo wa wasanii wa Kenya ambao watapata nafasi adimu ya  kupanda jukwaa moja na mastaa wa muziki kutoka Marekani la Boyz II Men watakaotumbuiza Jumamosi katika tamasha la Stanbic Yetu Festival katika bustani ya  Uhuru Gardens jijini Nairobi.

Tamasha hilo ambalo linaandaliwa kwa mara ya pili linafadhiliwa na benki ya Stanbic kwa ushirikiano na kampuni ya Radio Africa Group.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved