Jaji Mugure Thande aliyesimamisha kwa muda utekelezwaji wa Sheria ya Fedha ya 2023 Rais William Ruto ni miongoni mwa majaji 13 waliohamishwa katika mabadiliko ya hivi punde katika idara ya mahakama.
Mugure amehamishwa hadi Mahakama ya Malindi katika mabadiliko yaliyofanywa na Jaji Mkuu wa Mahakama kuu Jaji Eric Ogola. Nafasi yake itachukuliwa na Jaji Chacha Mwita, ambaye atakuwa Jaji mkuu katika Kitengo cha Katiba na Haki za Binadamu cha Milimani.
Mwita aliwahi kuhudumu Malindi hapao awali.Jaji Diana Kavedza ataongoza mahakama mpya maalum katika Mahakama za Kibra na Kahawa. Kwa sasa ametumwa katika Idara ya Uhalifu ya Milimani.
Jaji David Majanja amepelekwa katika Kitengo cha Kiraia kutoka wadhifa wake katika Kitengo cha Biashara na Kodi.
Katika mabadiliko hayo, Mahakama Kuu ya Nakuru itaongozwa na Jaji Hedwig Ong'undi wa Kitengo cha Katiba na Haki za Kibinadamu huko Milimani.
