logo

NOW ON AIR

Listen in Live

MP Peter Salasya aorodhesha sifa za mwanamke anayetaka kumuoa

Mbunge huyo mseja tangu achaguliwe katika uchaguzi amekuwa akidokeza kutafuta mke.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri25 March 2024 - 09:09

Muhtasari


• Aliwaomba wafuasi wake kumpa ushauri ama aoe mwaka huu au mwaka kesho.

PETER SALASYA

Mbunge wa Mumias ya Mashariki, Peter Salasya ameweka wazi kwamba yuko sokoni na anatafuta mwanamke wa kufunga ndoa naye.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Salasya alifichua kwamba amechoka kukaa mseja na anahitaji mwanamke mzuri wa kukaa naye katika ndoa, kwani maisha bila mke yanampa uhuru mwingi usio na tija katika maisha yake.

Aliwaomba wafuasi wake kumpa ushauri ama aoe mwaka huu au mwaka kesho.

“Je, nioe mwaka huu au mwaka ujao? Naomba unishauri. Nataka kuwa serious na maisha. Hii life bila wife inanipa uhuru sana ambao hauhitajiki sana,” Salasya alisema huku akionesha picha akiwa amebarizi kwenye kochi la kifahari nyumbani kwake.

Salasya alisonga mbele na kutaja baadhi ya vigezo na sifa ambazo anahitaji kutoka kwa mwanamke anayetaka kumuoa.

Salasya alisema kwamba hataki mwanamke anayekuja kwake na kuanza kumuongoza katika kila maamuzi na pia akaweka wazi kwamba anataka mwanamke ambaye atakubali kuishi kijijini kwao na wanaonana mara moja tu kwa mwaka.

“Nataka kuoa lakini sitaki mwanamke mwenye atanikalia chapati. Aniruhusu niwe naye mara moja tu kwa mwezi. Apende kukaa kijijini kuliko Nairobi. Naeza pata kweli?” Salasya aliuliza.

Mbunge huyo mseja tangu achaguliwe katika uchaguzi amekuwa akidokeza kutafuta mke.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved