logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Abiria kadhaa wajeruhiwa katika ajali kwenye barabara ya Mombasa

Majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Sultan Hammud Level 4 ambapo walikuwa wamelazwa na kupokea matibabu.

image
na GEORGE OWITI

Yanayojiri10 November 2024 - 12:59

Muhtasari


  • Hii ni baada ya gari walimokuwa wakisafiria kugongwa na trela katika eneo la Mlima Kiu hatua chache kutoka soko la Salama Kaunti ya Makueni.
  • Ajali ilisababishwa na trela lilokuwa likotoka Nairobi wakati ambapo lilikuwa linapita magari mengine katika mteremko hatari wa Salama.


Watu sita ambao ni abiria waliokuwa kwenye basi wakitoka Mombasa wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya umma ya sultan Hamud kaunti ya Makueni.

Hii ni baada ya gari walimokuwa wakisafiria kugongwa na trela katika eneo la Mlima Kiu hatua chache kutoka soko la Salama Kaunti ya Makueni kwenye barabara kuu ya Mombasa-Nairobi usiku wa kuamukia leo. 

Ripoti ya maafisa wa trafiki kutoka kaunti ndogo ya Mukaa zinasema ajali hii ilisababishwa na trela lilokuwa likotoka Nairobi wakati ambapo lilikuwa linapita magari mengine katika mteremko hatari wa Salama hivyo kugonga basi hilo upande mmoja na kupelekea ajali hii.

Majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Sultan Hammud Level 4 ambapo walikuwa wamelazwa na kupokea matibabu.

Eneo la tukio lilihudhuriwa na kushughulikiwa na maafisa wa trafiki kutoka kituo cha polisi cha Mukaa.

"Trela ​​lililokuwa likitoka Nairobi kuelekea uelekeo wa jumla wa Mombasa lilikuwa likiyapita magari mengine kwenye barabara kuu ya Nairobi - Mombasa eneo la Mlima Kiu wakati lilipogonga basi lililokuwa likielekea kwenye kisa cha ajali," afisa wa polisi alisema.

Mabaki ya magari yote mawili yalivutwa hadi kituo cha polisi cha Salama yakisubiri ukaguzi.

Kisa hicho kilisababisha msongamano mkubwa wa magari kwenye barabara kuu Jumapili asubuhi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved