logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua aendeleza shutma dhidi ya Rais William Ruto

Naibu rais huyo wa zamani amelalamikia kufifia kwa vita dhidi ya pombe haramu haswa katika eneo la mlima Kenya tangu aondolewe madarakani

image
na Brandon Asiema

Yanayojiri23 December 2024 - 07:43

Muhtasari


  • Gachagua amemtaka Rais kuacha hasira na kurejea kwa watu na kufanya mazungumzo namna alivyojitokeza na Bibilia wakati wa kampeni akiomba kura.
  • Gachagua amemlaumu rais William Ruto kwa kukosa kuendeleza kampeni dhidi ya pombe haramu tangu ang’atuliwe mamlakani huku akimshutumu kwa kuruhusu machifu na polisi kuacha kupigana dhidi ya pombe haramu


Naibu wa rais aliyeng’atuliwa mamlakani Rigathi Gachagua ameendeleza shutma dhidi ya rais William Ruto akimhusisha na matatizo yanayoshuhudiwa nchini shutuma za kurejea kwa pombe haramu ambapo watu watatu waliripotiwa kufa baada ya kubugia pombe katika eneo la Lanet, kaunti ya Nakuru.

Akizungumza katika ibaada ya kanisani mjini Naivasha, Gachagua amemlaumu rais William Ruto kwa kukosa kuendeleza kampeni dhidi ya pombe haramu tangu ang’atuliwe mamlakani huku akimshutumu kwa kuruhusu machifu na polisi kuacha kupigana dhidi ya pombe hiyo haramu haswa katika eneo la mlima Kenya.

Gachagua amemsuta rais kwa kuruhusu pombe haramu katika eneo la mlima Kenya jambo ambalo amelitaja kuwa nia ya kuwamaliza vijana na eneo hilo ili kupunguza idadi ya wapiga kura wa ukanda huo wa kati wa Kenya akitaja kuwa kinyume cha maadili na jambo lisilokubalika kulenga jamii.

“Tangu wanitoe kwa kiti ile pombe yote mbaya ya kuua watu rais aliagiza iletwe hapa kwa mlima imalize vijana wetu. Na ni kinyume cha maadili, ni jambo lisilokubalika kulenga jamii kwa uharibifu na sumu.” Alisema Gachagua katika ibaada ya kanisa la PCEA mjini Naivasha.

KiongozI huyo wa zamani katika utawala wa Kenya Kwanza, mbali na kulalamikia kulegea kwa vita dhidi ya pombe haramu, ameisuta serikali kwa kukosa kukamilisha miradi ya maendeleo kama vile usambazaji wa umeme, miradi ya ujenzi wa barabara na maji akitofautiana na miradi ya ujenzi nwa nyumba ya bei nafuu.



Mbunge huyo wa zamani wa Mathira aameshangazwa na namna Wakenya watafika kwenye nyumba hizo za bei nafuu ikiwa hamna miundo m,binu msingi ya usafiri ambayo ni barabara.

“Hakuna hata moja umemaliza, Barabara zimesimama, maji imesimama, stima imesimama wewe unasema unataka kujengea watu manyumba, sasa hii manyumba kama hakuna barabara watu watafika wakipitia wapi? Alisema Gachagua.

Hata hivyo Gachagua amemtaka Rais kuacha hasira na kurejea kwa watu na kufanya mazungumzo namna alivyojitokeza na Bibilia wakati wa kampeni akiomba kura.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved