Shule zinapofunguliwa kote nchini madarasa za kidato cha
kwanza yatasalia bila wanafunzi baada ya
mtaala mpya ya elimu ya CBC kushika kasi.
Shughuli za masomo zinaporejelea rasmi Jumatatu tarehe 6, Januari kwa mwaka 2025 historia itaandikwa ambapo hapatakuwepo usajili wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha kwanza kwa masomoya sekondari chini ya mtaala wa 8-4-4.
Wanafunzi ambao walikalia mtihani wao wa kitaifa katika mwaka wa 2023 walikuwa kundi la mwisho la 8-4-4 kufanya mtihani wa KCPE na kujuinga na shule ya upili, na pia watakuwa wa mwisho kumaliza cheti cha elimu ya sekondari ya Kenya (KCSE) mnamo 2027.
Serikali iko mbioni kutekeleza elimu inayozingatia umahiri (CBC) na kukomesha hatua kwa hatua mfumo wa 8-4-4 ulioanza mwaka 1985.
Mwaka mpya wa masomo unapoanza Jumatatu Januari 6, darasa la kwanza la CBC litakuwa linajiunga na daraja la 9. Awali, shule za sekindari ya chini zilikuwa zikimilikiwa na shule za sekondari lakini kufuatia malalamiko na kero zilizotolewa na wadau mbalimbali wa elimu ilichangia kusalia kwa junior sekondari katika shule za msingi.
Uchagizo huu umesababisha mabadiliko makubwa kwani shughuli za kurudi shuleni zimekuwa tulivu kuliko kawaida. Wazazi wachache wameripotiwa kuzuru madukani kutafuta vifaa kama vile sare, vitabu na vifaa vingine vilivyozoeleka kuhitajika na wanafunzi wa kidato cha kwanza.
Wachapishaji na maduka ya vitabu pia wanahisi matatizo ya kifedha. Awali, biashara hizi huona ongezeko la mauzo mwanzoni mwa mwaka wa masomo wanaposambaza vitabu muhimu vya marejeleo. Hata hivyo, mwaka huu, wanakabiliana na akiba isiyouzwa ya vitabu vya kiada vya kidato cha kwanza.
Taasisi ya ukuzaji mtaala ya Kenya (KICD) pia ilikanusha madai ya uhaba unaokaribia wa vitabu vya kiada, haswa kwa Darasa la tisa ikisistiza kuwa kuna idadi ya kutosha ya vitabu hata katika maduka.
Mwaka wa masomo unaahidi kuwa wakati mahususi katika mageuzi ya mfumo wa elimu wa Kenya, huku nchi ikikabiliana na mabadiliko ya mahitaji ya CBC.