logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waziri wa Teknolojia na mawasiliano William Kabogo amuajiri kazi Gen Z kwa jina Kennedy Maina kutoka Kiambu.

Waziri wa teknolojia na mawasiliano William Kabogo amemwajiri Gen Z kwa jina Kennedy Maina kutoka gatuzi la Kiambu hii inafuatia hatua yake ya kukejeli mradi wa Kabogo wa Wifi.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri31 January 2025 - 10:25

Muhtasari


  • Akiangika picha yake na ya  Maina  kwenye mtandao wake wa Facebook waziri Kabogo alisema kuwa anamhongera Maina kwa kujitolea kimasomaso na kuonyesha ukakamavu katika kuzungumzia suala hilo.
  • ''Hujambo ndugu jina langu ni Maina  kutoka gatuzi la Kiambu tumeona na kukusikia ukizungumzia kuhusu kutoa huduma za mradi wa WIFI ya bure .


Waziri wa teknolojia na mawasiliano William Kabogo amemwajiri Gen Z kwa jina Kennedy Maina kutoka gatuzi la Kiambu hii inafuatia hatua yake ya kukejeli mradi wa Kabogo wa WIFI ya bure kwenye masoko mbalimbali mtaani kwao, aliodai ni mradi ghushi na hautumiki kwa vyovyote vile.

Akiangika picha yake na ya  Maina  kwenye mtandao wake wa Facebook waziri Kabogo alisema kuwa anamhongera Maina kwa kujitolea kimasomaso na kuonyesha ukakamavu katika kuzungumzia suala hilo,vilevile waziri aliambatanisha arafa aliotumiwa na Kennnedy iliosheheni kejeli za kuusuta mradi huo wa WIFI  ambao alidai hautumiki kabisa.

Katika ujumbe wake bwana Kennedy alisema kuwa amekuwa akifatilia kwa ukaribu semi ambazo waziri amekuwa akisema kuhusu kutoa Mitambo hiyo ya WIFI bure katika masoko mbalimbali akisema kuwa haikuwa ikifanya kazi bali ni maneno matupu.

''Hujambo ndugu jina langu ni Maina  kutoka gatuzi la Kiambu tumeona na kukusikia ukizungumzia kuhusu kutoa huduma za mradi wa WIFI ya bure  katika masoko mbalimbali yaliyoanzishwa na serikali kwa bahati mbaya inaonekana tu kimuundo bali haitumiki wala kutoa huduma yoyote''.

Kabogo alipousambaza ujumbe huo alisisitiza kuwa Kennedy hakukashifu tu miradi yake bali alileta mwanga na mwamuko mpya ndio maana niliamua kumuajiri kazi,akasisitiza kuwa kauli ya Kennedy ilikuwa ni pevu tena ya kufungua macho hivyo alipoupokea ujumbe kutoka kwake alipendezwa na maoni yake Kabogo alipousambaza ujumbe huo alisisitiza kuwa Kennedy hakukashifu tu miradi yake bali alileta mwanga na mwamuko mpya ndio maana niliamua kumuajiri kazi,akasisitiza kuwa kauli ya Kennedy ilikuwa ni pevu tena ya kufungua macho hivyo alipoupokea ujumbe kutoka kwake alipendezwa na maoni yake na akaazimia kumwajiri papohapo.

''Wazo ambalo Kennedy alitoa lilikuwa ni wazo zuri akisema kuwa WIFI ambayo imeratibiwa kutumika na Umma au katika sehemu za umma yafaa itumike na mtu kwa kulipia kiwango cha hela anazo tofauti na WIFI ambayo hutolewa kwa kampuni mbalimbali ambazo huwa ni ghali sana kuzilipia''hili lilikuwa wazo la Kenney kwa waziri Kabogo ambaye katika mtazamo wake alikuwa ameazimia kuzima mitambo hiyo yote.

Kabogo alikiri kuwa wazo la Kennedy lilikuwa zuri na kama wizara sasa wanalenga kuimarisha utendakazi na kutekeleza kila jambo ili kila kitu kiwe sawa kwani hii ni hatua muhimu na kwa  hivyo wizara inapanga kuanzisha mradi mpana ambao utawajiri vijana wengi na kuimarisha hali zao za maisha hapa bwana Kennedy amenisalimi kwa uchanya 'nimesalimiwa positively' Kabogo alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved