logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC Yatangaza Maeneo Ya Kenya Ambako Stima Zitapotea Leo, Alhamisi

KPLC walisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarbati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo

image
na Samuel Maina

Yanayojiri06 February 2025 - 08:25

Muhtasari


  • KPLC  imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Februari 6.
  • Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni Tharaka Nithi na Kiambu.

caption

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Februari 6.

Katika taarifa ya siku ya Jumanne jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti mbili za eneo la Mlima Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

KPLC walisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarbati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni Tharaka Nithi na Kiambu.

Katika kaunti ya Tharaka Nithi, baadhi ya sehemu za maeneo ya Giampampo na Rukindu zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi unusu alasiri.

Sehemu za maeneo ya Kamwangi, Watathi, Mbichi, Wangige, na Gathiga katika kaunti ya Kiambu pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved