logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kaunti 12 Ambazo Zitaathirika Na Kukatizwa Kwa Umeme Leo, Jumanne - KPLC

KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumanne, Februari 18, 2025.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri18 February 2025 - 08:14

Muhtasari


  • KPLC imetangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti 12 za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.
  • Kaunti zitakazoathirika ni Nairobi, West Pokot, Uasin Gishu, Nandi, Kakamega, Homa Bay, Meru, Laikipia, Nyeri, Murang'a, Taita Taveta na Mombasa.

KPLC staff

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumanne, Februari 18, 2025.

Katika taarifa ya siku ya Jumatatu jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti 12 za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, West Pokot, Uasin Gishu, Nandi, Kakamega, Homa Bay, Meru, Laikipia, Nyeri, Murang'a, Taita Taveta, na Mombasa.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za maeneo ya Lang'ata Road, Kileleshwa, Dandora, Pipeline Estate na Amazon Pipeline zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Kapkoris na Chepareria katika kaunti ya West Pokot yataathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Outspan na Ancillia katika kaunti ya Uasin Gishu yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi alasiri.

Sehemu za maeneo ya Yala na Kaimosi katika kaunti ya Nandi zitakosa umeme kati ya saa tatu unusu na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Sigalagala na Musoli katika kaunti ya Kakamega yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za Oyugis, Nyangiela, na Ombek katika kaunti ya Homa Bay zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi alasiri.

Maeneo ya Maua na Garba-Tulla katika kaunti ya Meru yataathirika kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Timau na Embori katika kaunti ya Laikipia pia yataathirika kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi unusu alasiri.

Katika kaunti ya Nyeri, soko la Kiamabara litakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja asubuhi.

Maeneo ya Kenol na Kimorori katika kaunti ya Murang'a yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za mji wa Mwatate katika kaunti ya Taita Taveta zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.

Maeneo ya Fort Jesus, na Mombasa Hospital katika kaunti ya Mombasa pia yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved