logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC Yatangaza Maeneo Yatakayoathirika na Kukatizwa kwa Umeme Leo, Jumatatu

KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatatu, Februari 24.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri24 February 2025 - 08:03

Muhtasari


  • Kampuni ya KPLC ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyika kwenye mitambo.
  • Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Kajiado, Nyeri, na Meru.

KPLC staff

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatatu, Februari 24.

Katika taarifa ya Jumapili jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyika kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti tatu za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na Kajiado, Nyeri, na Meru.

Katika kaunti ya Kajiado, sehemu za maeneo ya Ngong VET zitakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Kinunga, Ihwa, Chania, na Soko ya Iruri katika kaunti ya Nyeri zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Soko ya Igoji na Soko ya Kinoro katika kaunti ya Meru pia zitaathirika kati ya saa mbili na nusu asubuhi na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved