logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IEBC yadai shilingi bilioni 61.7 kuandaa uchaguzi wa 2027

Keitany mnamo siku ya jumanne Februari 25,2025 alisema IEBC itahitaji shilingi bilioni 61.7 za uchaguzi

image
na Evans Omoto

Yanayojiri26 February 2025 - 09:34

Muhtasari


  • Keitany alielezea kamati kuwa tume inalenga kuwasajili wapiga kura wapya 5.7 kufikia mwaka wa 2027.
  • Tume hiyo ya IEBC huhitaji jumla ya makamishina saba akiwemo  afisa mkuu mtendaji wa tume .

IEBC itahijaji kitita cha shilingi 61.7bilioni kwa ajili ya kuandaa uchaguzi wa 2027, Obadia Keitany alisema

Kaimu afisa mkuu mtendaji wa IEBC Obadia Keitany siku ya jumanne Februari 25,2025 alisema IEBC itahitaji shilingi bilioni 61.7 kwa ajili ya uchaguzi wa 2027.

 Alipofika mbele ya Kamati ya haki  na sheria  katika bunge la taifa alielezea kuwa tume inalenga kuwasajili wapiga kura wapya 5.7 kufikia mwaka wa 2027 ambapo idadi hiyo itawezesha jumla ya wapiga kura kuwa 28m.

IEBC inapojianda kuteua makamishina wapya watakaojianda kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao mamia ya wakenya walionyesha ari ya kutaka nafasi hiyo na kufikia sasa jumla ya watu 1848 walituma maombi ya kuhitaji kazi hiyo.

Itakumbukwa kuwa mnamo mwaka wa 2021 aliyekuwa mwenyekiti wa IEBC marehemu Wafula Chebukati alikuwa amependekeza kupewa shilingi bilioni 40.9 ili afanikishe uchaguzi ulio huru na wahaki wa mwaka wa 2022.

Wakati huo huo tume inapojianda na kuhakikisha kuwa makamishina wanateuliwa na jopo kazi lililoteuliwa na hatimaye kuapishwa baada ya kupigwa msasa na bunge la taifa watalazimika kuwa wepesi wa kufanya kazi ikizingatiwa kuwa muda uliosalia ni mchache kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao.

Kufikia sasa jumla ya shilingi milioni 481 zilikwisha tengwa  kwa ajili ya kushughulikia chaguzi ndogo katika sehemu mbalimbali ambazo Wabunge,Madiwani,Mavana, Maseneta na Wawakilishi wa kina mama kwa ajili ya kushughulikia chaguzi ndogo kutoka maeneo hayo.

IEBC inapojianda na kuratibu mipango na mikakati ya uchaguzi mdogo na ujao  rai zinazidi kutolewa kwa tume hiyo kupewa muda mwafaka ofisini ili kuwe na umakinifu na mafunzo ya kutosha kwa makamishina watakaoteuliwa.

Tume hiyo ya IEBC huhitaji jumla ya makamishina saba akiwemo  afisa mkuu mtendaji wa tume ambaye pia hutumika ka sekritari wa tume.

Kumekuwa na shinikizo nyingi kutoka kwa Wakenya na Viongozi kwa kutaka tume hiyo iunndwe kwa wepesi ili kurahihisha shughuli za uchaguzi na kutimiza matakwa  ya Katiba bila kuingia katika migogoro ya  kikatiba  na kuvunjwa kwa sheria.

Kucheleweshwa kuundwa na kuwateua makamishina wa IEBC kulitokana na kesi zilizokuwa zimewasilishwa  kortini kuzuia mchakato huo kuanza hadi kesi zisikilizwe na kuamuliwa, lakini mapema mwaka huu korti iliondoa vizingiti hivyo na kuruhusu mchakato rasmi kwanza.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved