logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Geoffrey Mosiria afafanua Chanzo cha uhasama wake na Babu Owino

Alipokuwa akihojiwa na kituo Kimoja nchini Bwana Mosiraa aliweza kufafanua kuwa tofauti zao zilianza pale walipokuwa katika chuo kikuu

image
na Evans Omoto

Yanayojiri17 March 2025 - 12:13

Muhtasari


  • Mkuu wa Kitengo cha Mazingira katika Kaunti ya Nairobi bwana Geoffrey  Mosiria alielezea sababu kuu ambayo uhasama kati yake na Mbunge wa Embakasi Mashariki  Babu Owino ulipoanzia.
  • Alifafanua kuwa Mheshimiwa Babu kwa mara si moja ameishi kwa misemo kuwa hamna siku ambayo atawahi kuja kushindwa au kuwa mtu kando na kuwanianafasi ya kiti cha uongozi  katika chuo kikuu.

Mkuu wa Kitengo cha Mazingira katika Kaunti ya Nairobi bwana Geoffrey  Mosiria alielezea sababu kuu ambayo uhasama kati yake na Mbunge wa Embakasi Mashariki  Babu Owino ulipoanzia.

Alipokuwa akihojiwa na kituo Kimoja  nchini Bwana Mosiraa aliweza kufafanua kuwa tofauti zao zilianza pale walipokuwa katika chuo kikuu cha Nairobi .

Alifafanua kuwa Mheshimiwa Babu kwa mara si moja ameishi kwa misemo kuwa hamna siku ambayo atawahi kuja kushindwa au kuwa mtu kando na kuwanianafasi ya kiti cha uongozi  katika chuo kikuu.

Bwana Mosira aliendelea na kusema kuwa alishindana na babu Owino lakini aliibiwa Kura katika chuo kikuu cha Nairobi.

‘’Uhasama wangu na Babu ulitoka mbali ,Babu huwa anaamini kuwa mimi sitawahi mshinda kwa vyovyote vile kando tu na kuwania siasa za vyuoni ama sitawahi Kuwa chochote, Nilishindana na Babu katika kura za kusaka uongozi chuo cha Naoirobi.

Kutokana na Babu kuwa alikuwa amejulikana na uongozi wa  chuo sana aliweza kuibiwa kura na  na kutangazwa mshindi  aidha mkuu wa Kaunti ambaye amepata umaarua mwingi katika Mitandao ya Kijamii kutokana na hatua  yake ya kusuluhisha majanga   yanayotokana na  Mazingira .

Alifafanua akisema kuwa alisema kuwa Babu alimtafuta kumwarifu kuwa alikuwa na azma ya kuwania kiti katika eneobunge la Embakasi Mashariki mwaka wa 2017.

Kulingana na Mosira chama cha ODM kilimtaka asimame ili aweze kutwaa ushindi wa chama hicho Alisema kuwa katika uchaguzi uliofuata vilevile alimtafuta ambapo waliketi katika mkahawa mmoja sehemu za Kileleswa ili kuzungumzia masuala ya  siasa.

‘’Bwana Owino alinirai kwa sababu mimi ni binadamu nilimuelewa na kumpa kibali cha kuendelea’’ Bwana Mosira aliendelea kufafanua kuwa huwa anamwogopa  akidhani kuwa huwa anadhani kuwa anapana  kuwa mpinzni wake mkuu katika kinyan’ganyiro cha kusaka uongozi wa  eneo bunge la Embakasi Mashariki.

Bwana Mosira alionekana kumushauri Babu Kutekeleza wajibu wake kama mbunge kwa kuhakisha kuwa anawapa wananchi waliomchagua maendeleo ya  kudumu na badala yake aache kuingilia kazi za huduma za usafi wa Kaunti kwa kutuma takataka katika mitandao malimbali ya kijamii kuashiria kuwa kazi haifanywi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved