logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilimpa kila MCA 20m za maendeleo waulize walifanyia nini - Otuoma

Otuoma alikuwa anazungumza baada ya kuhudhuria ibaada.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri17 March 2025 - 12:50

Muhtasari


  • Paul Otuoma ni gavana wa sasa na wa pili wa kaunti ya Busia.
  • Akizungumza amewataka wawakilishi wadi kuwa tayari kubeba msalaba wao siku ya kiama itakapofika.

Paul Otuoma, Current governor of Busia County
Gavana wa Kaunti ya Busia Paul Nyongesa Otuoma sasa anasema kwamba aliwapa wawakilishi wadi wote wa kauniti hiyo shilingi milioni 20 kila mmoja za kufanya maendeleo katika wadi zao.

Otuoma ambaye alikuwa anazungumza baada ya kuhudhuria ibaada alionekana kumujibu mbunge wa Funyula oundo  mudenyo baada ya kutilia shaka utenda kazi wake.

"Nataka kusema bwana Oundo, sisi hapa pesa tunapeana kwa wodi, ukieka words zote pamoja inashindana na yenye mnapata ya CDF. Sasa wakati mwingine hata mimi nashindwa, badala ya mwakilishi wadi kutembea akiambia wananchi nimepewa pesa fulani na kwa wodi yangu nafanya hii, wengine ni kuongea juu ya Gavana,' alisema Otuoma.

"Kwa mfano hiyo pesa uchukue kama hapa Samia kama ziko wadi nne, tayari hiyo ni milioni 80, pamoja na zile tunaongeza ni zaidi ya shilingi milioni 100. Pesa ambazo zinatoshana na za mgao wa Usitawi wa maeneobunge CDF. Sasa badala wewe useme umefanya nini kwa wadi yako, mbunge akisema amefanya nini na wewe pia unasema umefanya nini, " alieleza

Vile vile akizungumza amewataka wawakilishi wadi kuwa tayari kubeba msalaba wao siku ya kiama itakapofika iwapo watashindwa kueelezea wenyeji kile ambacho watakuwa wamekifanya kwa miaka mitano.

"Kila mtu kwa wodi yake atahesabu kazi yake wala sio kulaumu gavana, siku ya kiama ikifika kila mtu atajitetea. Kwa sababu nimepeana bilioni mia saba kwa wawakilishi wadi wote kwa pamoja na hizo ni pesa nyingi sana. Hakuna sheria ambayo inasema nafaa kuwapatia hiyo pesa. Mlifanya kampeni mkiahidi na tumewapea mtimize," aliweka wazi Otuoma.

Paul Otuoma ni gavana wa sasa na wa pili wa kaunti ya Busia.

Alichaguliwa kuwakilisha eneo bunge la Funyula katika Bunge la Kenya tangu uchaguzi  mwaka 2007 na alikuwa waziri wa serikali za mitaa kuanzia 2010-2013. Alikuwa Mbunge wa Jimbo la Funyula hadi Agosti 2017.

Otuoma ni daktari wa mifugo aliyehitimu akishikilia Shahada ya Tiba ya Mifugo kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi (1991), ambapo pia alipata MBA mnamo 2001.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved