Aliyekuwa Gavana wa Meru aliyebanduliwa Mamlakani Kawira
Mwangaza alivunja kimya chake kwa mara ya kwanza tangu uamuzi wa korti
ulipotolewa wa kumuondoa afisini.
Mnamo Ijumaa ya Machi ya tarehe 14,2025 mahakama kuu
iliweza kuafikiana na uamuzi wa Seneti wa kumbandua Mwangaza kama uliafikia viwango vyote vya Kisheria.
Akizungumzia hali yake ya kuondolewa mamlakani siku ya
Jumanne ya tarehe 18 Machi,2025 kupitia kwa mtandao wake wa Facebook Mwangaza aliweza kumtaja aliyekuwa Gavana
wake Bwana Mutuma M’ethingia kama kibaraka mkuu na ambaye alitumika kufanikisha
malengo ya mahasidi wake kisiasa.
Aidha aliweza kusema kuwa kuondolewa kwake kulichochewa
na viongozi ambao ni wanasiasa wakuu walioshinikiza kubanduliwa kwake mamlakani.
Alisema kuwa kuondolewa kwake kulitokana na yeye kutokubaliana na viongozi madalali ambao walikuwa na azma ya kupora na kuvuja mali ya umma kwa njia ya ufisadi akisema kuwa yeye hakuwa na wakati wa kuwapa sikio wala nafasi hiyo hivyo walizuumu kumuendea bwana Mutuma ambaye waliweza kumshawishi na kumtumia kama Daraja.
Aliweza kusema kuwa kutokana na msimamao wake mgumu wa
kuhakikisha kuwa usawa, haki na sheria inafuatwa kwa kila jambo ni baadhi ya sababu kuu zilizochochea maadui zake kumpiga
vita kwani inasemekana walitaka mtu ambaye alikuwa wa kushawishika upesi.
Kwa upande mwingine viongozi walionekana wakimsifia Bwana
Mutuma kwa kumtaja kama kiongozi ambaye kulingana na wao ni kiongozi ambaye
hukaa afisini na kutia sahihi stakabadhi mbalimbali.
Kwa upande mwingine
Bi Kawira aliweza kutajwa kama kiongozi ambaye hakukuwa anachukua muda wake
mwingi kukaa afisini wala kutia sahihi
stakabadhi mbalimbali bali alionekana akiwa mashinani kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo jambo
ambalo halikuwafurahisha wengi.
‘’Ajenda kuu haikuwa kuhusu maendeleo na miradi ya Meru bali
ilikuwa ni kuniondoa afisini kwa sababu wapinzani wangu walihisi nitawabwaga
katika uchaguzi ujao wa 2027 kutokana na historia yangu ya maendeleo katika
Kaunti hii ya Meru nimechapa kazi bila uwoga’’ Mwangaza alisema
Mwangaza kabla awe Gavana alikuwa mwakilishi wa kike wa
Meru ambapo alianza kupalilia uongozi wake ifaavyo na akauchukua Ugavana wa
Meru kama muaniaji Huru akiwabwaga washindani wake wa karibu Kama Kiraitu Murungi
na Mithiika Linturi.