
Shabiki mmoja wa mpira alilalama baada ya gari lake kuibiwa kutoka mahali alikokuwa ameliegesha.
Mlalamishi alisema kuwa alikuwa ameliegesha gari lake kando ya barabara ya Kisauni nyuma ya hospitali ya Nairobi, alipokuwa akitazama mechi Kati ya Harambe star na Gabon ugani Nyayo.
Aliporipoti katika kituo cha Polisi cha AKILA mlalamishi aliweza kusema kuwa aliegesha gari lake IST lenye nambari ya usajili KBN 093B lenye rangi ya shaba saa 3:40pm na akafululiza hadi kwenye uwanja kulipokuwa na mashabiki wa kushabikia mchuano wa soka.
Akisimulia masaibu yake ya kupoteza gari vilevile na timu ya taifa Harambee star kupoteza kwa kupigwa mabao mawili kwa moja baada ya mchezaji Aubameyang kuwaweka Gabon Kifua mbele kwa magolo 2-1, alisema jioni ya saa moja alirudi kulichukua gari lake akapata haliko.
Baada ya kuwasilisha stakabadhi zote na kuonyesha kuwa gari lili,opotea lilikuwa lake, gari hilo limeweza kutangazwa kote kama gari lililoibiwa na maafisa wa DCI kutoka kituo cha Langata hivyo kuruhusu msako mkali dhidi yake.
Kwingineko katika eneo la JuJa uchunguzi wa kina unaendelea kutafuta aina mojawapo ya Gari lililoibiwa TOYOTA AXIO lenye Usajili KCR 628U ambalo liliibiwa kutoka mtaa wa Matangi karibu na shule ya msingi ya Kimbo.
Mwenye gari alikuwa ameliegesha gari hilo katika mahali pake pa maegesho mtaani ila alipoamukia asubuhi hakulipata wala kuliona jambo ambalo lilimuacha akiwa amechanganyikiwa na akiwa na msongo wa mawazo.
DCI iliweka wazi nambari za mawasiliano ili kuweza kusaidia katika shughuli ya uchungiuzi na kupatikana kwa magari hayo yote yalioyoibiwa , nambari ya kupigaripoti kwa polisi ni 999911112 au 0800722203 ikitumia kauli kuwa Fichua kwa DCI.
Kulingana na DCI uchunguzi wa kina unalengwa kuanzishwa ili kuhakikisha kuwa magari hayo yanapatikana na walioyaiba wanakamatwa na kufunguliwa mashitaka kulinganna na mjibu wa sheria , hata hivyo umma umeibua hali ya wasiwasi kutokana na ripoti nyingi za wizi wa magari kila uchao hio ikiashiria kuwa wanancghi wengi wataanza kuhofia kuegesha magari katika maegesho ya umma kwa sababu ya ukosefu wa usalama wa kutosha.
