logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Noordin Haji NIS na Charles Kahariri wa KDF wazungumzia hali ya usalama wa taifa

Asasi muhimu za usalama kitengo cha usalama wa kijasusi nchini NIS na Jeshi la ulinzi la taifa KDF zatoa taarifa kuhusu usalama wa taifa

image
na Evans Omoto

Yanayojiri28 March 2025 - 08:32

Muhtasari


  • Noordin Haji ambaye ndiye  mkurugenzi mkuu katika  kitengo cha ujasusi nchi(NIS)  aliweza kuelezea umuhimu wa  kuwahusisha wananchi ipasavyo katika masuala ya Usalama wa Taifa.
  • Alisema kuwa haki ya wananchi ya kupinga au kususia mambo kutoka kwa utawala ulioko madarakani ni haki ya kila mmoja kutekeleza ila akasisitiza kuwa jambo hilo ni lazima litekelezwe kwa mujibu wa katiba.

Asasi  muhimu za usalama nchini  NIS na Jeshi la ulinzi la taifa  zimeelezea umuhimu wa  kuwahusisha wananchi ipasavyo katika masuala ya Usalama wa Taifa. 

Kulingana na mujibu wa  maelezo ya bwana Haji alisema kuwa kukosekana kwa usalama kwa taifa kwa namna moja au nyingin kunaweza leta hali tete katika jamii na  hata  kuhatarisha Biashara za  watu jambo ambalo si  zuri.

Alisema kuwa haki ya wananchi ya kupinga au kususia mambo kutoka kwa utawala ulioko madarakani ni haki ya kila mmoja kutekeleza ila akasisitiza kuwa jambo hilo ni lazima litekelezwe kwa mujibu wa katiba.

'' Kama kitengo cha ujasusi nchini tuna wajibu wa kuhakikisha kuwa tunawafahamisha na kulinda usalama wa nchi kwa manufaa yetu sisi sote, Katika kufanya hivyo tunahakikisha kuwa tunatekeleza haya masuala  kwa uwazi  na kwa kushirikisha umma ambao ni washikadau muhimu katika idara ya usalama kwa jumla.'' Sehemu ya  hotuba ya  Noordin ilieleza.

'' Kama ilivyo ada na desturi habari za ujasusi  huweza kutekelezwa kwa usiri sana kwa kushughulikia habari ambazo hazifai kuwekwa wazi kwa  umma  hivyo kujenga na kuimarisha mifumo imara ya usalama wa  taifa kwa kuhakikisha kuwa usalama wa wananchi na biashara zao zinatekelezwa kwa mazingira  ambayo ni salama''.

Alisema kuwa usalama ni nguzo munhim ya taifa  hivyo basi ikiwa  kutatokea jambo lolote ambalo linakisiwa kuweza kuhatarisha maisha  ya wananchi bila shaka ni jukumu la  Ujasusi kuweza kuingilia kati kwa  haraka.

'' Jinsi tujuavyo  masuala ya ujasusi kama ilivyo ada   hutekelezwa kwa usiri ila yanapotekelezwa kwa usiri haimanishi kuwa ni dhaifu, tunafahamu fika kuwa katika enzi hizi za utandawazi  watu  hupinga mambo ambayo hawakubaliani nayo ila ni lazima kutokubliana huko kuwe ndani ya misingi ya  sheria, watu hutaka habari, majina na maelezo ya kile wanachokitaka'' sehemu ya hotuba ilisimulia.

Aliweza vilevile kusungumzia hali ya usalama katika taifa la Sudan Kusini kwa kusema kuwa kama taifa wako mstari wa mbele  kuhakisha kuwa  mataifa jirani yanakuwa salama kwa ushirikiano na mataifa yenye nia njema kama Misri, Chad, na Ethiopia hata  hivyo aliweza kuzungumzia kuhusu matumizi ya mitandao katika kukabili usalama wa taifa na wa mataifa  mengine.

 Kwa upande mwingine Komanda  wa jeshi la taifa Bwana Charles Kahariri aliweza kuelezea msimamo wao kama jeshi kwa masuala ya taifa  na siasa akisema kuwa jeshi huwa halina muegemeo wowote wa siasa na kusema kuwa hata kama Wakenya wanapinga utawala uliopo ni lazima  watekeleze kwa kuzingatia  katiba.

''Tunapaswa kuafikiana na kuelewana na uongozi uliopo badala ya kushinda tukisema ''Must GO'' ni lazima tufanye hivyo kwa kuangazia sheria sio tu kusema na ilihali nyinyi ndio mliomchagua kila kitu kifanywe kwa kuangazia sheria za taifa''. Kahariri alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved