
Wizara ya afya ilisisitiza kuwa utekelezaaji wa kitaifa wa elimu ya hali za ujana katika masuala ya ngono kwa vijana ililenga kuimarisha ujana wao na kuwapa ufahamu mwema.
Wizara ilisema kuwa ilikuwea mbioni kuhakikisha kuwa inawalinda vijana dhidi ya kuambukizwa maradhi kutokana na maradhi yanayotokana na kushiriki mapenzi.
Kanuni hizo zilianzishwa miaka mitatu iliyopita zikilenga kupunguza vita na mizozo ya wapenzi ikiwemo na kutekeleza mambo ya ubakaji pamoja na kupata mimba za mapema wizara ilidokeza.
Daktari Jacqueline Kisia mkurugenzi kuhusu masuala ya uzazi alisema wizara iliweza kuangazia umuhimu wa kuangazia ukubwa wa historia ya afya na tathimini yake kwa jumla.
Katika kuangazia usambazaji huo asilimia 15 ya watoto walio na umri wa miaka 10-18 walikuwa wamejifungua . Aliweza kusisitiza kuwa kama wizara walikuwa wanafanya hima kuhakiksha kuwa namba hio inapungua na akasema kuwa ''watoto hawasitahili kuwa wanapata watoto.'' katika umri wao huo mdogo.
Alikuwa akizungumza na wanahabari kuhusu hamasisho jijini Nairobi chini ya kauli mbiu maalum ya '' step up to access''kampeini.
Daktari Christine Wambugu anayesimamia idara ya ujana na rika alisisitiza kuhusu umuhimu wa uhusiano mwema kati ya wazazi na watoto wao ili kujadili masula ya vijana na kuwaeleza athari za kushiriki mapenzi katika ujana mdogo.
Alisema kuwa wizara ilikuwa wazi kuzindua mikakati faafu na bainifu kuhusu uwazi kuhusu masuala ya mapenzi .
Hata vivyo kibabu maalimu kuhusu masula na mapenzi na ujana kilichapishwa ili kuweza kuwapevusha vijana pammoja na walezi kuhusu masuala ya maopenzi.
Kuhusu mpangilio huo na utaratibu huo maalumu uliopigiwa upato na mpango wa vijana kutangaza masuala ya upatikanaji wa mimba za mapema miongoni mwa vijana kama jambo ambalo lilikuwa lafaa kushughulikiwa kwa uwazi na kwa umakini sana.
Ni kampeni ambayo ililenga mataifa ya Kenya,Uganda,Malawi,Zimbabwe na Zambia ambapo kampeni hio ililenga kuhamasisha vijana kuhusu mimba za mapema na jinsi ya kujitunza.
Afisa mtendaji kuhusu magonjwa ya vizusi vya Ukimwi Tandale Songore aliweza kusisitiza umuhimu wa kuelimisha na kuwapa mwanga wa ufahamu kusuhu mabadiliko yao ya mwili na jinsi ya kujikinga na kuelewa mabadiliko katika miili zao.
Vilevile afisa huyo aliweza kuelezea kuwa habari hizi na ujumbe huo unalegwa kuhakikisha kuwa unawaafikia wanafunzi katika shule mbalimbali kote nchi.